MUONYESHE HESHIMA NA SHUKRANI
jifunze kuwa na shukrani hata kwa mambo ma­dogo anayokufanyia, Hata kama ame kununulia pipi, au kama mwenzi wako amekupa zawadi au kitu ambacho hujakipenda, muonyesha shukrani kwanza alafu ndio umuonyeshe hujakipenda.

KUWA NA MUDA WA KUMCHUN­GUZA NA KUMUELEWA
Unatakiwa umchunguze akiwa na hasira anakuwa­je na akiwa na furaha anakuwaje, ana­penda sana kufanya mambo gani (hobi) au anapenda sana zawadi za namna gani. Ukishamjua, ni rahisi sana kuishi naye hata pale anapokasirika au ana­pokerwa na jambo fulani.

Jishushe na kuwa na utaratibu wa kumuomba msamaha unapokosea ila usiombe msamaha kama hujakosea, Bila kujali kwamba wewe ni mwa­naume au mwanamke, mkubwa au mdogo, una fedha au huna, inapotokea umeziumiza hisia za mwenzio,ni lazima uombe msamaha na kuahidi kutorudia makosa.

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz ,twiter@edonetz ,inst@edonetz_blog na youtube@edone tv
 
Top