Banana Zorro awataja wasanii wa Bongo Flava anaowakubali kwa kuimba live
 
Ukiambiwa utaje orodha ya wasanii wa Bongo Flava waliobobea kwenye muziki wa live, huwezi kuacha kumtaja Banana Zorro.
Muimbaji huyo anayetoka kwenye familia ya muziki – baba yake akiwa Mzee Zahiri Zorro, gwiji wa muziki wa dance, Banana amejikusanyia weledi na uzoefu mkubwa wa kuimba live kupitia bendi yake, B Band.
Na sasa akiongea na mtangazaji wa Kings FM, Prince Ramalove, muimbaji huyo wa Nzela amewataja wasanii wawili wa Bongo Flava anaowakubali kwa kuimba live. Wasanii aliowataja ni Barnaba na Ruby.
Wawili hao licha ya kuwa na uwezo katika kuimba muziki jukwaani, kwa sasa wanafanya vizuri redioni na nyimbo zao ‘Lover Boy’ na ‘Walewale’ huku Ruby akidaiwa kufanya maajabu kwenye msimu mpya wa Coke Studio Africa.
Kwa upande mwingine, Banana amekiri kuwa muziki wa live unazidi kukua Tanzania, kitu anachosema alikuwa akikipigania kwa kipindi kirefu.

Dully Sykes, amekuja  kivingine na tour ya Dar ‘kwa mara ya kwanza atakuwa na mabaunsa’
 
Msanii wa muziki anayefanya vizuri na wimbo ‘Inde’ Prince Dully Sykes amejipanga kuja kivingine katika tour yake jijini Dar es salaam ambayo itaanza weekend hii Club 71.
Akiongea na Bongo5 Alhamisi hii, Dully amesema ameamua kufanya baadhi ya mabadiliko kwenye team yake ili kuonyesha utofauti wa Dully wazamani na huyu wa sasa.
“Mikoani mambo yalikuwa mazuri sana namshukuru Mungu na sasa ni zamu ya Dar es salaam,” alisema Dully “Tour yangu ya Dar itaanzia Club 71. Kutakuwa na surprise zakutosha, pia Dully nitakuja kivingine nikiwana na mabaunsa, kwa sababu huyu pia ni Dully mpya ambaye anahitaji usalama kwenye show zake,”
Muimbaji huyo amesema katika show hiyo atasindikizwa na wasanii ambao atawaweka wazi hapo baadae.

Sam wa Ukweli aitaja Al Jazeera ndiyo walionizima

 
Msanii wa Bongo Flava aliyetamba na wimbo ‘Sina Raha’ Sam wa Ukweli amefunguka na kutoa sababu iliyomfanya akae kimya kwa kipindi kirefu.
Muimbaji huyo amesema kuwa lebo yake ya Al Jazeera ndiyo iliyosababisha awe kimya kwa muda mrefu.
amesema alitaka kuvunja mkataba na lebo ya Al Jazeera kutokana na kuona hakuna kazi iliyokuwa inafanyika, hivyo alitaka kuwa huru lakini ilishindikana na aliambiwa alipe shilingi milioni 100 kama anataka kutoka kwenye lebo hiyo, hali hiyo ilinifanya akae kimya kwa muda mrefu.
Muimbaji huyo ameongeza kuwa mkataba wake na lebo hiyo umeshamalizika na sasa yupo tayari kufanya kazi na mtu yoyote.


Kala Jeremiah ameleza kwanini mwaka huu hana mpango wa kuachia albamu
 
Msanii wa muziki wa hip hop Kala Jeremiah amefunguka na kusema kuwa mwaka huu hana mpango wa kuachia albamu mpya kutokana na kazi kubwa ambayo aliifanya katika albamu yake iliyopita.
Kala amesema albamu yake iliyopita bado inaendelea kumpatia mshavu mpaka sasa.
amesema kweli kazi ambayo aliifanya kwenye albamu yake iliyopita ilikuwa ni kubwa sana, albamu  ilikuwa na nyimbo 23,” Hata msanii afanye vipi hawezi kuachia nyimbo 23 ndani ya mwaka mmoja hata miwili kama ukiamua kuachia wimbo mmoja mmoja, kwa hiyo yeye anajua bado albamu yangu ina muda wakutosha kwa wananchi, mwaka huu hana mpango wa kuachia albamu,
Rapa huyo alisema albamu hiyo bado inaendelea kumpatia mashavu mbalimbali katika muziki wake kwa kuwa hiyo ni CV ambayo anatembea nayo katika maisha yake ya muziki.
Kala kwa sasa anafanya vizuri na wimbo ‘Wanandoto’ ambao aliutoka miezi miwili iliyopita.


Msami ameeleza sababu za kuachana na Irene Uwoya
 

kama wewe utakuwa ni mpenzi wa kufuatilia mahusiano ya mastaa basi penzi la Mrembo kutoka Bongomovie (Irene Uwoya) na Mkali kutoka Bongofleva (Msami)  litakuwa sio kitu kigeni kwenye macho yako sasa leo   Msami ameweka wazi sababu za kuachana na Ireen Uwoya
‘amesemakuachana kama kuachana mimi sioni kama tumeacha kwasababu mimi na Ireen bado tunawasiliana sema tu mimi niliona kuna vitu haviendi sawa nikaamua kukaa pembeni yaani sina sababu maalumu ila niliamua tu mwenyewe.” Maneno ya msami…

Bobby Shmurda aenda miaka saba jela
Baada ya kukubaliana na upande wa mashtaka, rapper Bobby Shmurda kutoka Brooklyn, amehukumiwa kwenda jela miaka saba Jumatano hii.
Mwezi uliopita, Bobby alikiri mashtaka ambayo yaliyokuwa yanamkabili ya kumiliki silaha kinyume cha sheria. Shmurda aliambia mahakama kuwa alilazimishwa na mwanasheria wake kukubali hukumu hii ili asihukumiwe miaka mingi zaidi.
Mwanzo alikuwa amehukumiwa miaka 5 lakini alikuwa hajakubali kwasababu rafiki yake, Chad “Rowdy Rebel” Marshall alikuwa amehukumiwa miaka 12 kwahiyo ikabidi aongezewe ili rafiki yake apunguziwe. Wote wamehukumiwa miaka 7 na mahakama.


Jaffarai  hataki kufanya kolabo na mastaa, anataka kuwasaidie wasanii wachanga
 
Msanii mkongwe wa muziki, Jaffarai, amesema kuwa hataki kufanya kolabo na mastaa bali atakuwa anafanya kolabo na wasanii wachanga ili kuibua vipaji vipya.
Rapa huyo ambaye yupo mbioni kuachia wimbo mpya hivi karibuni, amesema kuwa alikuwa kimya ili kupisha shughuli za fiesta ambazo zinaendelea.
Kwamba Kuna kazi mpya inakuja, ni kolabo na msanii na mchanga kabisa, mimi sitaki kufanya kolabo na mastaa,” alisema Jaffarai.
Aliongeza,yeye ni msanii mkongwe, kuna namna nyingi ya kuwasaidia wasanii wachanga kwa kufanya nao kolabo, kwa hiyo yeye anasema mashabiki wakae mkao wa kula kwa ajili ya kazi mpya,”
Wimbo wa mwisho kuachia rapa huyo ulikuwa ni ‘Wakati’ ambao alimshirikisha Kassim Mganga.

Jennifer Lopez aungana na NBC kutengeneza series mpya
 
Kituo cha runinga cha NBC kimeungana na Jennifer Lopez kutayarisha tamthilia iliyopewa jina C.R.I.S.P.R.
C.R.I.S.P.R.— ambayo ni kirefu cha ‘clustered regularly interspaced short palindromic repeats’ ni tamthilia ya kisayansi.
Hiyo haitakuwa mara ya kwanza NBC inafanya kazi na Jennifer. Wameshirikiana kwenye tamthilia Shades of Blue. Lakini pia Lopez atatayarisha na kuwa jaji wa mashindano ya kucheza ya World of Dance.
Pamoja na NBC, Lopez ana mradi wa tamthilia ya sheria na CBS huku pia akitarajiwa kucheza kama muuza unga, Griselda Blanco kwenye filamu ya TV ya HBO.
Bondia Dulla Mbabe kuzipiga na Mchina Dar 28 Oktoba
Bondia kutoka Tanzania Dulla Mbabe anatarajia kupanda ulingoni tarehe 28/2016 mwezi Oktoba, kupambana na Bondia Chengbo Zheng kutoka Taifa la China Pambano la WBO litafanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
Mwandaaji wa pambano hilo Jay Msangi amesema mshindi wa pambano hilo atajinyakulia Mkanda wa ubingwa, huku pia kukiwa na mapambano mengine mengi ya utangulizi ambayo yatawakutanisha mabondia kutoka Tanzania na nje ya Tanzania.

Jay Msangi ameongeza kwa sasa wataandaa mapambano mengi ya kimataifa kwa mabondia wa Tanzania kwa lengo la kuwandaa kufuzu mashindano ya Olimpiki nchini Japan.
 
Top