Karibu sana msomaji wa edonetz katika mada ya leo ili tujuzane juu ya hili la leo ikiwa ni kuzungumzia mahusiano tuanzie hapa.

Upo uhusiano ambao umelengwa kudumu, hasa kwa wanandoa.  Kuna wengine hawana sura ya kudumu, wapo kwa muda kwa kuzingatia mazingira pamoja na kile kilichomo ndani ya nafsi zao.
Unaweza kujiuliza; Kwa nini ufike wakati utake kuvunja uhusiano wako na mwenzako? Iwe wa
kirafiki au kimapenzi, Ipo wazi kwamba kuna sababu mbalimbali zinazoweza kuwafanya wahusika kuamua.

Yawezekana uhusiano wako na mpenzi au rafiki yako wa jinsia tofautiikiwa unaona anakutia hasara, au anakuharibia biashara, au unakupunguzia heshima katika jamii, au pengine uaminifu wako kazini 
Mathalan, mpenzi wako anafahamika kuwa ni
kahaba. Inawezekana uhusiano wako na mwenzako unaidhuru nafsi yako. Mfano, mwenzio ana nguvu sana juu yako kiasi kwamba huwezi kusema “hapana” kwa lolote analokwambia. Pengine kutokana na hali hiyo umekuwa ukilazimika kufanya mambo ambayo huyapendi na ambayo hayaendani na maadili.

Lakini pia yawezekana umeanza kumchukia mwenzako.  Mazingira yamebadilika, kwa hiyo wewe na yeye hampatani tena. Unajitazama na kugundua kwamba ulivyo huendani naye. Ni matokeo ya kuchokana!
Uhusiano wowote unapoyumba, uwe wa kirafiki au kimapenzi, huwaweka wahusika katika wakati mgumu kiasi kwamba ni lazima mmoja achukue hatua ili aweze kuishi kwa amani na furaha ya kweli.

Hata hivyo, ikae akilini kwamba inauma mno kuachana na mtu unayempenda! Kumaliza uhusiano wa kimapenzi au kirafiki si hatari, lakini la msingi ni kuhakikisha kuwa unamwacha mwenzako akiwa hajaathirika kisaikolojia kwa namna yoyote.


Kwa leo naishia hapo lakini ukigundua baadhi ya vitu kama hivyo chukua hatua ndugu.. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top