SIO kitu kigeni katika maisha ya kila siku kukumbana au kukutana na watu wenye matatizo haya ya kukoroma haijarishi ni mwanaume au mwanamke na hili ni miongoni mwa vitu vinavyochokera kupita maelezo ni pale inapotikea unalala na mtu anayekoroma. ASEE Inakera kweli kweli kwani kelele za mtu anayekoroma hukosesha wengine kufaidi raha ya usingizi kwa sababu ukweli ni kwamba ukiachilia mbali raha ya kujinyoosha pia usingizi una raha yake asikwambie mtu;

Basi inapotokea mtu akakukatisha raha hiyo huwa tafrani tupu. Watu wengi wana tabia ya kukoroma wanapolala, lakini kukoroma siyo kuzuri sana kwani familia yako pengine hushindwa kupata usingizi vizuri kutokana na makelele yanayotokana na kukoroma kwani maana halisi ya kukoroma kunamaanisha kuwa pumzi zako haziko sawa, wataalamu wa masuala ya afya wanasema wakati mtu anapokoroma kunaweza kusababisha kukosa pumzi na kupelekea kifo.

kumbuka  mtu anaekoroma mwili wake haupati mapumziko ya kutosha na mara nyingi huamka huku bado akihisi uchovu na husababisha watu wengine kunenepa sana na wengine kukonda ikitegemea mwili wa muhusika na homoni zake.
Tatizo hili linaweza kuisha  kabisa baada ya wiki 2 unatakiwa kuendelea  na mazoezi hata mara mbili kwa wiki ili misuli isilegee tena.
ZINGATIA YAFUATAYO…

Kwa hivyo, zifuatazo ni ‘tips’ kadhaa zitakazokusaidia kubadilisha hali hii.

·       Kwanza kuchagua mito laini inayoweza kufanya shingo yako iwe vizuri, ambayo itakusaidia kupumua vizuri.

·       Pili tumia mashine ya (humidifier) ili hewa ndani ya chumba iwe ya unyevu na kukusaidia koo lako kutokuwa kavu.

·       Tatu, kunywa asali kidogo kulainisha koo lako na usinywe pombe kwani inapandisha shinikizo la damu na kuwa juu hivyo kusababisha  koo lako kubana na kuzuia kupata pumziNne, ambalo ndilo jambo la msingi kabisa linalosisitizwa na wataalamu wa afya ni kufanya mazoezi mara kwa mara ! Mazoezi ni dawa iliyothibitika kutibu magonjwa mengi.

FANYA ZOEZI HILI ITAKUSAIDIA SANA..
Fungua mdomo wako mpaka mwisho, toa ulimi na usukume nje mpaka mwisho,rudisha ulimi ndani mpaka mwisho-rudia mara 20.

Ukimaliza utahisi kuna misuli nyuma na pembeni ya koo umeifanyisha kazi,sasa misuli hii ikilegea ndio inayosababisha kukoroma.Fanya zoezi hili mara 2 mpaka 3 kwa siku na tatizo hili litaisha baada ya siku 10-20 kutegemea mtu hadi mtu.

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top