Ukiongelea vitu vitamu zaidi duniani lazima utaje na asali ambayo inatengenezwa na wadudu aina ya nyuki ambao wanachanganya vitu mbali mbali kama ifuatavyo…
Asali  hutengenezwa na nyuki wanaotumia vumbi’ maalum la maua liitwalo nectar.  Kiwango cha sukari katika asali ni asilimia 70 hadi 80 na kiasi kinachobaki ni maji, madini na huwa na kiwango cha protini, asidi na vitu vingine.
Asali imekuwa ikitumika kwenye matibabu ya vidonda, matatizo ya ngozi na magonjwa tofauti ya tumbo na ina uwezo wa kuua bakteria mwilini. Pamoja na uzuri na utamu wa asali lakini pia ina madhara yake kwani inaweza kuongeza uwezekano wa kutokwa damu, ikiliwa pamoja na dawa zinazoyeyusha damu kama vile Asprini, dawa za kuzuia damu kuganda kama Warfarin (Coumadin), Heparin na kadhalika.
Asali pia inaweza kushusha kiwango cha sukari mwilini, hivyo lazima kuwe na tahadhari ya matumizi yake kwa mtu mwenye ugonjwa wa kisukari anayetumia dawa zinazoshusha sukari mwilini kwa sababu zikitumika kwa pamoja huweza kusababisha kushuka sana kwa kiwango cha sukari na kuleta hatari ya kifo au kifafa kwa mtumiaji.
Asali pia inaweza kuingiliana na dawa zinazofanya kazi kwa kutumia kimeng’enya mwili cha Cytochrome p450 kinachofanya kazi  ya kuvunja dawa na hivyo huweza kufanya dawa ifanye kazi kwa kiwango kidogo ama kufanya kazi kwa kiwango zaidi ya kile kilichokusudiwa hivyo kuwa sumu ama kutomsaidia mtu.
Inashauriwa mtumiaji wa dawa hizo aonane na mtaalam wa afya ili amueleze kama ni salama kunywa dawa zinazohitaji kimeng’enya hiki katika utendaji kazi mwilini pamoja na asali kwa usalama wao.

Asali pia inaweza kuingiliana na dawa za damu, moyo, mfumo wa ufahamu, ngozi, tumbo au matumbo, fangasi, mfumo wa mkojo, saratani, kifafa, kupunguza lehemu, meno, pombe, kupunguza uzito na dawa za kutibu vidonda. Asali pia inaweza kushusha shinikizo la damu mwilini, hivyo wagonjwa wanaotumia dawa za kushusha shinikizo la damu la juu (High Blood Pressure), wanapaswa kushauriana na madaktari wao kabla ya kutumia. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top