Watafiti wa masuala ya mahusiano na ndoa wana kalenda za miaka ya hatari iliyotafsiriwa sambamba na sababu zinazoweza kuvuruga uhusiano na kuwafanya watu waliokuwa wakipendana kuachana.
Hivyo kwa dondoo tu nimeona ni vyema nikudadavulie watu wanaoishi kwenye ndoa sababu zinazotafsiri ukomo wa mapenzi yao kulingana na miaka husika iliyotafsiriwa na watalaamu wa masuala ya ndoa na mahusiano.
Wanasaikolojia mbalimbali ulimwenguni kupitia tafiti zao walikubali kuuweka UGOMVI  kuwa katika sababu zinazoweza kusababisha ndoa kuvunjika ndani ya mwaka 1-2. Wanasema endapo watu waliooana wakianza kugombana kati ya mwezi wa kwanza na kuendelea, basi ujue kuwa wanandoa hao hawawezi kuvuka miaka miwili kabla ya ndoa yao kuvunjika.
Jambo la kuzingatia katika sababu hiyo ya ugomvi iliyotajwa ni kwamba watafiti hao hawachukulii hitilafu na migongano ya kawaida kama sababu, bali mikwaruzano mikubwa yenye kuumiza mwili au roho kwa kiasi kikubwa.
Watafiti hao wanasema wanandoa na wapenzi hugombana kwa kipindi hicho huwa na kasoro ya ulinganifu wa tabia, mawazo na mwelekeo hivyo kuwafanya wasiweze kuishi pamoja kwa muda mrefu.
Hivyo ili wanandoa wasiweze kuachana katika miaka miwili ya mwanzo wanashauriwa kuoana baada ya kuchunguzana vema tabia na kulingana katika hali.
Mwaka mwingine wa hatari ni wa NNE. Baada ya kuoana mwaka wa nne unatajwa na watafiti kuwa ni wa hatari katika kuwafikisha wapendanao ukingoni mwa mapenzi yao.
Sababu ambayo  inapewa uzito katika kizuizi hiki cha ndoa ni kufanikiwa kupata MTOTO. Kuwekwa kwa mtoto katika kizingiti hiki kunaonekana na tafiti nyingi kuonesha kuwa wanandoa wanapofanikiwa kupata mtoto hujisahau na kuhamisha mapenzi yao kwa mtoto, huku wakijisahau kuwa wao pia wanajukumu la kupendana.
Watafiti hao wanasema wapendanao wanapokuwa na mtoto, muda mwingi humfikiria zaidi yeye. Kama ni suala la kuchukua zawadi za kurudi nazo nyumabani hazitakuwa kwa ajili ya mume/mke bali itakuwa ni kwa mtoto.

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW

fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top