Uchunguzi kuhusu madini na jiografia ya sayari ya Mars unaonesha katika zama za kale sayari hii ilifanana na dunia tunamoishi na ilikuwa na maji mengi. Lakini swali linalogonga vichwani mwa wengi ni je, viumbe viliwahi kuishi kwenye sayari ya Mars? Na vipi hadi sasa bado kuna viumbe vinavyoishi kwenye sayari hiyo yenye ukame mkubwa? Jibu la maswali haya limepatikana kupitia utafiti mpya uliotolewa kwenye Gazeti la Nature Communications kwamba ukame mkubwa umekomesha maisha yote na kuifanya Mars iwe sayari yenye mazingira mabaya kwa viumbe hai.
Katika miaka bilioni 3 iliyopita, Mars ilikuwa na bahari, mito na maziwa na inafaa kwa maisha ya viumbe lakini sasa imebadilika na kuwa sayari yenye ardhi nyekunduKikundi cha wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Stirling huko Scottland kimetafiti mazingira ya hivi sasa ya Mars. Kiongozi wa kikundi hicho Dk. Christian Shroder amesema hivi sasa ukitaka kutafuta dalili ya viumbe kwenye sayari hii, unatakiwa kutafuta mapango yenye kina kirefu ambayo yapo mbali na ukame na mionzi.

Kikundi hiki kimetafiti muda wa madini ya chuma kupata kutu kwenye Mars. Muda huo unahusiana na kuwepo kwa maji. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa muda huo kwenye Mars ni mara 10 hadi 10,000 ya muda huo kwenye jangwa lenye ukame mkubwa zaidi katika dunia yetu. Hii inamaanisha kuwa ukame umeendelea kwa mamilioni ya miaka kwenye sayari hii. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top