Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya mapenzi, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.

Watu wengi wamejikuta kwenye kashfa za kuitwa wahuni kwa kubadilisha wanaume/wanawake kwenye maisha yao kwani wataalamu wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.

·kutambua vigezo vya mwenza wako unaye muhitaji;

kwa kila mwenye mwenza wake inabidi ujue mahitaji ya nafsi yako kwa kujua nini unataka kwenye mahusiano yako kwani watu wengi hawana elimu ya kutosha kuhusu mahusiano ndo mana unaambulia kuhangaika mara kwa bwana Juma mara kwa hasani au kwa upande wa wanaume ndo wanabadilisha sketi kam misemo ya vijana wa sikuizi.

·Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo.

Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.

·Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka; 

Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.

·Ushirikishaji wa ndugu;

Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. mtembezi.com  inakushauri usipuuzie maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana.

·kuzungumzia ufanyaji mapenzi,

hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.

·kutimiza ahadi ya Ndoa;


kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.


JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top