Virusi vya ukimwi vikianza kushambulia mwili hujionyesha na dalili kadhaa mwanzoni lakini pia dalili hizo huja kulingana na hatua nne kuu ambazo shirika la afya duniani lilikaa na kuzipanga baada ya kufanya utafiti wa mda mrefu..
Ugonjwa huu ambao unashambulia sana kinga ya mwili huja na hatua na dalili zifuatazo kama ilivyotajwa.
 
HATUA YA KWANZA.
Kuvimba kwa tezi zote za mwili.
                         
HATUA YA PILI
Kupungua uzito chini ya asilimia kumi bila sababu maalumu.
Kuugua mara kwa mara magonjwa ya kifua
Fangasi za kwenye ngozi na kucha.
Mkanda wa jeshi
Kuwashwa sana ngozi
                     
HATUA YA TATU
Kupungua uzito kwa zaidi ya asilimia kumi bila sababu yeyote.
Kuharisha bila sababu zaidi ya mwezi mmoja..
Fangasi za mdomoni
Kifua kikuu.
Upungufu wa damu
Magonjwa ya mdomoni mfano gingivitis..
Homa za mara kwa mara.
                   
HATUA YA NNE..
Kukonda sana ..
Fangasi za koo la chakula..
Kuchanganyikiwa kiakili.
Kansa ya ngozi mfano karposis sarcoma
Kupungua na kuharibika kwa uwezo wa mishipa ya fahamu..
Kuharisha zaidi na zaidi.
upofu wa macho
                   
Kumbuka, mgonjwa akishahamia kwenye hatua Fulani harudi nyuma ataendelea na hatua za mbele. Moja ya vigezo vya mgonjwa kuanzishiwa dawa za kurefusha maisha ni kufikia hatua ya tatu au ya nne, mgonjwa mjamzito na mtoto mdogo.

Watu wengi wakisoma makala kama hizi wanafikiri ukimwi ni watu Fulani lakini naomba nikwambie msomaji ukimwi upo Na unaua…. japokua ukifuata utaratibu wa matibabu utaishi maisha marefu na ya kawaida kama wengine. 

Hivyo unashauriwa kujizuia na ukimwi kama inavyotangazwa kila siku, kupima mara kwa mara na kuanza matibabu haraka kama tayari umesha athirika. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top