Pamoja na mwamko mkubwa wa kushirikiana katika kazi
za nyumbani kati ya mama na baba, bado mwanamke ana dhima kubwa
kuliko mwanaume. Nakumbuka mwanamke wa kwanza kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Magreth
Thacher aliwahi kukiri hadharani kuwa pamoja na majukumu makubwa ya
kuendesha nchi, alipokuwa nyumbani alikuwa akifanya kazi za nyumbani. Hata,
alikuwa akimpikia na kumwandalia mumewe chakula.
Wale
wanawake walikubaliana kuwa ulimwengu wa sasa umebadilika sana kwa pilikapilika
na misukosuko. Siyo kama ule wa zamani ambapo mama zetu na bibi zetu waliweza
kulea watoto hadi sita, wakapika vyakula vitamu, wakafanya usafi wa nyumba,
wakafua marundo ya nguo kwa mikono yao, wakasenya kuni na kuteka maji kwa
kichwa.
Pamoja
na yote hayo waliweza kutengeneza vifaa vya nyumbani kama kufinyanga vyungu,
kusuka mikeka na kujenga vihenge vya kuhifadhia nafaka. Vilevile waliweza kushiriki
katika shughuli za kijamii na burudani kama kucheza ngoma.
Lakini
katika maisha ya leo, ambapo wote mume na mke wanafanya kazi na wana watoto
kadhaa wanaowalea wenye ratiba yao pekee ya mambo ya shule na nyumbani.
Kutokana na yote haya hawana budi kukabiliana na maisha ya leo yenye changamoto
nyingi. Wanandoa wote hususan mwanamke atagundua kuwa katika maisha yake
anapungukiwa muda wa kutosha kufanya mambo yote yanayompasa. Siku ina saa 24 na
haziwezi kuongezeka. Tena, karibu saa nane za muda huo hutumika kwa usingizi.
Hizo saa 16
zinazobaki huwa haiwezekani kutumika zote kwa kazi. Utafiti umebainisha kuwa
kwa wastani mtu hupoteza karibu miaka tisa ya uhai wake kwa kufanya shughuli
zisizo na tija yoyote.
Shughuli hizo ni kama kukaa kwenye foleni
benki, posta na kwengineko; kusimama barabarani kungojea taa za waenda kwa
miguu, kutafuta watu kwenye simu, kwenye mikutano isiyo na tija na mengine
kadhaa wa kadhaa ya jinsi hii.
Leo
tuangazie baadhi ya mambo yanayoweza kumsaidia mwanamke kujipanga kuzifanya
kazi kwa utaratibu ulio sahihi zaidi na kuepuka matumizi mabaya ya muda mchache
alionao katika siku.
Kuweka malengo
na vipaumbele
Hii ni
hatua ya kwanza kabisa ambayo mwanamke anapaswa kuitumia katika kufanya kazi
huku akiyafanya maisha yake yawe ya raha. Akumbuke kuwa mambo anayopaswa
kuyafanya nyumbani na kwa familia yake ni mengi sana na hawezi kuyamaliza yote.
Hivyo
anatakiwa kila siku kufikiria mambo yote unayotakiwa kuyafanya. Kisha ujiulize
yapi yanaweza kusubiri na yapi hayawezi kusubiri. Hatimaye aorodheshe yale
anayopaswa kuyatimiza katika siku fulani na ayapange kufuatana na umuhimu.
Ayatekeleze kwa kuzingatia vipaumbele katika siku juma na hata mwezi.
Kutumia vifaa vya kurahisisha kazi
Katika
ulimwengu wa leo wa sayansi na teknolojia kuna zana na vifaa vingi vinavyoweza
kumsaidia mwanamke katika kudhibiti utekelezaji wa mangilio wa kazi, kutumia
vyema wakati na kurahisisha kazi zake. Baadhi ya zana hizo ni hizi zifuatazo:-
• Kulenda: Kalenda
ya ukutani au mezani ni zana muhimu katika kumkumbusha mambo muhimu unayotakiwa
kufanya katika mwezi. Mwanamke aliye makini katika shughuli zake huweza hata
kuwa na kalenda ndogo katika mkoba wake. Kalenda zake zitakuwa zimechafuka kwa
kuziwekea maelezo yake.
• Saa: Saa ya
ukutani na mkononi ni rafiki wa mwanamke anayejali wakati na aliye makini
katika kazi zake. Watu wengi husahau kuwa ni muhimu kuwa na saa mbele yake
anayoitazama kwa urahisi wakati wote ili kuchunga matumizi ya muda. Licha ya
kuwa saa kazini na nyumbani ni muhimu mwanamke awe na saa hata jikoni.
• Kijitabu cha
kumbukumbu: Mwanamke wa kisasa analazimika kuwa na kijitabu kidogo
cha kuandika mambo mbalimbali kama yale anayotakiwa kuyafanya katika siku.
Vijitabu hivi huwa na tarehe. Jambo alilopanga kulifanya siku fulani
asipolitekeleza siku alihamishie katika ukurasa wa siku inayofuata. Jambo
ambalo limehamishwa zaidi ya siku mbili aanze kulindika kwa wino mwekundu ili
kumtahadharisha kuwa limechelewa kutekelezwa.
• Vikaratasi vya
kubandika kwa
ajili ya kumbukumbu: Katika maduka ya
steshenari huuzwa vipande vidogo vidogo vya karatasi vyenye gundi upande mmoja
vinavyoweza kubandikwa katika sehemu mbalimbali. Hivi vinatumika kwa kuandika
mambo ambayo mtu amepanga kuyafanya kisha anakibandika mahali ambapo atakiona
wakati wote ili kulikumbuka jambo hilo.
Kwa kuwa
huwa vina rangi mbalimbali mwanamke anaweza kuamua rangi fulani kwa kazi za
aina moja na rangi nyingine kwa kazi za aina nyingine. Hivi anaweza kuvibandika
sehemu mbalimbali ili kumkumbusha kama vile ukutani, kwenye friji, gari na
kwingineko.
• Kikokotozi: Hiki ni
kimashine cha kufanya hesabu ambacho ni muhimu mwanamke wa kisasa awe nacho
anapoandaa bajeti ya matumizi ama anapokwenda kununua vitu dukani. Ahakikishe
kila wakati anacho katika mkoba. Kwa bahati siku hizi simu za mkononi zina
vikokotozi.
• Mafaili ya
kutunzia nyaraka: Hivi ni vifaa muhimu sana kwa mwanamke wa
kisasa. Atakuwa na faili kwa nyaraka mbalimbali muhimu kama vile bili za maji,
umeme, uzoaji wa takataka, kodi ya nyumba na vinginevyo. Pia kuna nyaraka
nyingne muhimu kama hati za kuzaliwa watoto wake, mkataba wa bima ya afya,
stakabadhi za ununuzi wa vitu vikuu nyumbani kama TV, Friji, Radio, Jiko n.k.
mwananchi
Zipo nyingi
ila endelea kufuatilia edonetz niaendelea kukuletea mada hii.
JIUNGE
NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz , twiter@edonetz , inst@edonetz_blog na youtube@edone tv