Image result for faida za maharage mwilini
Kwa mujibu wa utafiti mbalimbali, maharage, hasa meusi ni chanzo kizuri cha kirutubisho aina ya faiba kinachoshusha kiwango cha kolestro mwilini. Vilevile kiwango cha faiba kilichomo kwenye maharage meusi, huweza kudhibiti kiwango cha sukari kisipande haraka baada ya chakula, hivyo kufanya maharage kuwa lishe nzuri kwa wagonjwa wa kisukari na shinikizo la juu la damu.

Iwapo utapata mchanganyiko wa maharage meusi na ule mchele ‘mweusi’ ambao haujakobolewa na kuondolewa virutubisho vyake muhimu brown rice, basi utaweza kupata kiasi kikubwa cha protini na faiba ambacho huwezi kupata kutoka katika chakula kingine.
Image result for faida za maharage mwilini
Utafiti wa muda mrefu uliofanywa na jarida moja lijulikanalo kama Journal of Agriculture and Food Chemistry, unaonesha kuwa mbali ya maharage kuwa na kiwango kikubwa cha faiba, pia maharage yana virutubisho vingine vinavyojulikana kama Anthocyanins ambavyo hutoa kinga mwilini Antioxidant. Kiwango cha virutubisho hivyo kilichomo kwenye maharage, kinaelezwa kuwa ni kikubwa kuliko hata kinachopatikana kwenye matunda kama zabibu ambayo inaaminika kuwa na kiwango kikubwa zaidi.


Pia watafiti walipofanya tathmini ya ziada kwenye maharage, waliweza kubaini kuwa maharage yanapokuwa meusi zaidi, ndivyo ambavyo kiwango kikubwa cha kinga kinavyoweza kupatikana, yakifuatiwa na maharage ya rangi nyekundu, kahawia, njano na mwisho meupe. Hii ina maana kwamba maharage meusi ndiyo yana virutubisho vingi zaidi kuliko maharage meupe na rangi nyingine.
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv

 
Top