Image result for kitunguu saumu

Kitunguuvsaum kimekuwa kikitumika kutibu na kuboresha afya ya mwili
na hivyo kumfanya mtumiaji awe mrembo na mwenye afya bora.

Matumizi ya kitunguu saumu kibichi yamekuwa yakisaidia vitu vingi sana mwilini.

Baadhi ya hayo ni pamoja na kupambana na virusi, bakteria, fangasi na pia sumu mbalimbali hasa zile zinazosababishwa na baadhi ya vyakula mwilini.

Kutokana na hilo, matumizi ya kitunguu saumu kama tiba na kipodozi, ni jambo linalopendekezwa na wataalamu wa urembo wa asili.
Katika matumizi yake kitunguu saumu hutumika kwa kula na wakati mwingine kupaka, ambapo hili hutegemea zaidi na mahitaji au matatizo ya mtumiaji husika.

Pamoja na njia hizo nilizotaja hapo juu, lakini wataalamu wanashauri ulaji wa kitunguu saumu kibichi kila siku, kwani husaidia kuboresha afya ya muhusika.

Ikiwa utashindwa kukitafuna chenyewe, unaweza kuchanganya kwenye chakula kingine ambacho unatumia alimradi tu ukipate kikiwa halisi.
Kwenye urembo, kitunguu saumu husaidia kuondoa matatizo yafuatayo;
Chunusi

Changanya kitunguu saumu kilichosagwa kijiko kimoja na kijiko kimoja cha juisi ya ndimu. Chukua pamba na paka sehemu zote zilizoathirika. Kaa na mchangyiko huo kwa muda wa dakika 15 hadi nusu saa.Ikiwa utaendelea kwa muda wa wiki moja. Tatizo la chunusi litakuwa limeondoka kabisa.

Kunyonyoka kwa nywele
Ni kwa muda mrefu sasa kitunguu saumu kimekuwa kikitumika kama tiba ya kunyonyoka kwa nywele. Unachotakiwa kufanya ni kutumia mafuta yake kwa kupakaa kwenye ngozi ya kichwa kila siku kabla ya kulala.

Fanya hivyo mara kwa mara kwa muda usiopungua miezi mitatu na utaona matokeo yake. Ikiwa utakosa mafuta yake, si vibaya ikiwa utatumia kitunguu chenyewe kilichosagwa kwa kupaka kwenye ngozi ya kichwa kila siku usiku na kuosha asubuhi yake.


Fangasi vidoleni
Kupambana na fangasi kwenye vidole vya miguu na mikono, unashauriwa kutumia kitunguu saumu kilichosagwa kwa kupaka eneo lililoathirika. Hakikisha unakaa nacho usiku kucha ukiwa umevaa soksi ama glavu. Fanya hivyo kila siku hadi utakapoona muwasho na maumivu yameisha.


MBA
Paka kitunguu saumu kilichosagwa katika ngozi ya kichwa ama sehemu yeyote iliyoathirika. Hakikisha unatumia hadi pale ugonjwa utakapokuwa umetoweka kabisa.


 JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv 
 
Top