Image result for ask questions in class
Hakuna mtu ambaye ameshawahi kuishi bila kusema uongo kabisa.. kitaalamu mtu akiulizwa swali akajibu uongo, hali ya mwili hubadilika yaani mapigo ya moyo hukimbia, presha hupanda na anaweza hata kutokwa jasho. Kuna kipimo cha polygraphy ambaho hutumia njia hii kufahamu kama mtu anadanganya au vipi kwa kuangalia mabadiliko ya mfumo wa mwili pale anapokua anaulizwa maswali, mara nyingi kipimo cha polygraphy hutumika na askari polisi
Image result for ask questions in class
Sasa leo nitakujuza jinsi ya kujua mtu, rafiki yako, ndugu yako, mpenzi wako kama anakudanganya kwa kuangalia vitu muhimu wakati wa kumohoji.

Kitu cha kwanza ni kuchelewa kujibu swali;

yaan ukimuuliza mtu swali akachelewa kujibu kuna uwezekano mkubwa anadanganya lakini inategemea na aina ya swali ulilolo muuliza.

Pili ni kukosekana mahusiano ya maneno na vitendo; 

kwa hali ya kawaida mtu akiulizwa swali na akatakiwa kujibu ndio au hapana kama ni ndio atatikisa kichwa kwenda juu na kama sio kweli atatikisa kichwa kwa pembeni sasa mtu akiulizwa swali akadanganya ataenda tofauti na hali ya kawaida hapo utaona kwamba ulimi wake unakubali lakini mwili wake umekataa.

Tatu ni kukohoa kidogo au kumeza kabla ya kujibu; 
mtu akipata wasiwasi baada ya kuulizwa kitu ambacho kimemkosesha amani kitaalamu mfumo wa mishipa ya fahamu kama sympathetic pathway unakua umefanya kazi hivyo mate yatakauka mdomoni na kwenye koo hivyo kuondoa hiyo hali atakohoa kidogo au kumeza mate kabla hajajibu ili kupata muda zaidi wa kutafuta cha kudanganya.

Nne ni kuficha macho au mdomo kwa kutumia mikono;

hii hutokea bila yeye kufahamu kitaalamu kama subconcious level yaani kibinadamu anashindwa kuuvumilia ule uongo anaosema hivyo atajikuta mwenyewe anaweka mikono sehemu hizo bila kujua ila wewe unayemuuliza maswali ndio utagundua kwamba anadanganya.

Tano ni kushika shika sana sehemu za kichwa chake; 
mfumo wa sympathetic system ukianza kufanya kazi mishipa ya damu huanza kujikunja hasa na sehemu zinazokosa damu kama usoni huanza kuwasha kwa mbali na kua tofauti hivyo muongo atajikuta anakuna pua, anakuna sikio na hata viganja vya mikono.

Sita ni kuhangaika mazingira yanayomzunguka;
mtu anayedanganya akiulizwa swali anaweza kuanza kuanza kurekebisha vitu ambavyo viko sahihi kwa mfano kurekebisha tai,miwani, kuchomekea vizuri...

kama ni mwanamke muongo ataanza kuweka nywele vizuri na kurekebisha sketi yake kabla ya kujibu kumbuka kama akifanya vitu hivyo baada ya kujibu sio muongo au unamuuliza mtu swali amekaa mezani ghafla kila kitu kimebadilika sehemu kilipokuwepo yaani kahamisha glass ya maji, funguo zake, simu na kadhalika.

Saba ni kushindwa kukuangalia usoni; 
Unaweza ukaanza kumuuliza vitu vya kweli kabisa huku mnaangaliana lakini ghafla chomeka swali la tofauti ambalo unataka kujua kama ni kweli au sio kweli basi utaona anaanza kungalia pembeni na kushidwa kuangalia usoni na wakati mwingine kijasho chembamba kitamtoka.

Lakini nane ni kua na maneno mengi sana; 
unaweza ukampigia simu ukamuuliza mtu kwamba yuko wapi akakujibu nilienda hospitali kuona mgonjwa nimechoka sana ntajitahidi leo nilale mapema nk... mtu wa  huyu anaweza kua medanganya kitu sasa anajaribu kukificha na maneno mengi ili usimjue lakini ukute kwa hali ya kawaida angesema niko hospitali kisha akakaa kimya.

Tisa ni kupunguza sauti; 
mtu kama ukianza  kumuuliza mambo anayofahamu kwa uhakika mfano jina lake, miaka yake, anaishi wapi au kama ni mchumba wako unaweza kumuuliza rafiki yake anaitwa nani, anafanya kazi gani na hapo atakua mchangamfu na kujibu vizuri kisha ghafla ukamuuliza nasikia umelala na mwanaume fulani hapo sauti itakua ndogo na atakataa kwa sauti ya chini.

Mwisho kabisa ni kuapa mara nyingi;

Mtu muongo hujitahidi sana kujitetea aonekane hana kosa yaani kila baada ya muda ata apa kwa mungu, atakua na kauli kama 'ukweli kutoka moyoni".

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top