Papaya mealybug ni mdudu mdogo anaefyonza majimaji ya kwenye kwenye safu ya nje ya majani , matunda na shina na anaingiza sumu ambayo inapelekea kubadilika rangi kuwa njano kwa mmea ,kudumaa , kufanya mmea ukose umbo maalumu ,kufanya majani na matunda yadondoke yakiwa 
machanga na kufanya mmea kufa.                                                
wadudu hawa wanapendelea kukaa kwenye mafungu na muonekano kama wa pamba juu ya mmea na wanatoa nta.                                       hutoa asali ambayo huziba matundu ya kutolea hewa kwa mmea na kusababisha mmea kushindwa kujitengenezea chakula chake. 
Wadudu hawa hutambaa mmea mmoja kwenda mwingine na kusababisha kuenea kusambaa ,wanaenezwa kwa kirahisi na upepo ,maji ,ndege ,mchwa , wanyama, wanadamu ,nguo ,na vifaa.
wadudu hawa waweza zuiwa kwa kuondoa mchwa ,kukagua mara kwa mara ili kutambua uwepo wao ,kuondoa magugu ,kuondoa mabaki ya mmea ,kusafisha vifaa kabla.
 
Top