Ufuta (simsim/sesame) ni zao la kibiashara ambalo mbegu zake zina kiasi kikubwa cha mafuta kiasi cha asilimia 45 hadi 55.Na zao hili linaweza kulimwa maeneo mengi ya Afrika mashariki na Tanzania.Ni zao ambalo linatowa mafuta yenye thamani kubwa na hivyo kulifanya zao bora la biashara.

Ufuta ni zao linalolimwa kwa wingi katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Pwani, Morogoro, Dodoma, Tanga na ukanda wa chini katika mikoa ya Rukwa na Mbeya. Zao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mbegu za zao hili huwa na wastani wa mafuta kiasi cha asilimia 45.

Kwa sasa soko la ufuta Tanzania ni zaidi ya mara tatu ya uzalishaji wake, kwa mantiki hiyo zao hili lina soko kubwa sana. Uzalishaji wake unafanyika kwa kiasi kidogo kwa sababu wakulima wamekuwa wakilima zao hili la ufuta kwa mazoea na kutumia mazao yake kama nafaka ya kutengeza vyakula mbalimbali kama kashata. Lakini kama utalima kibiashara ni zao ambalo linaweza kukomboa jamii yetu kutoka katika dimbwi la umasikini.

HALI YA HEWA INAYOFAA KWA KILIMO CHA UFUTA
Zao hili linawezwa kulimwa katika maeneo yanayopata mvua kidogo. Maeneo ya ukanda wa chini usawa wa bahari hufaa zaidi kwa kilimo cha ufuta. Pia nyanda za juu ambazo ni chini ya mita 1500 hufaa kwa kilimo cha ufuta. Mfano kwa Tanzania unaweza Ukalima ufuta katika mikoa ya Morogoro,Lindi,Manyara,Dodoma,Iringa.

UDONGO UNAOFAA KWA KILIMO CHA UFUTA
Ufuta ustawi vizuri katika maeneo yenye udongo mwepesi mweusi na usiotuamisha maji,udongo tifutifu ni mzuri kwa kilimo cha ufuta,Pia ufuta unawezwa kulimwa katika udongo wowote lakini usiotuamisha maji.Ufuta hufa haraka kama maji yatatuama kwa muda mrefu shambani.

AINA ZA UFUTA
Kuna aina kuu mbili za mbegu za ufuta:
1) MBEGU ZA ASILI - Wakulima wengi hupanda mbegu za asili, mbegu ambazo zilianza kulimwa miaka mingi iliyopita.Mbegu hizi nyingi zina mavuno kidogo na huchukua muda mrefu kukomaa Huchukua siku 140 hadi 180.

2) MBEGU ZA KISASA - Mbegu hizi zinakomaa kwa muda mfupi na hutowa mavuno mengi, wastani wa kilogram 500 hadi 800 kwa ekari kama shamba litaandaliwa litapandwa na litatunzwa vizuri.Mbegu hizi huchukua siku 105 hadi 140 kukomaa.Mfano wa mbegu hizi ni Naliendele 92,Lindi 202,Ziada 94 na Mtwara 2009.

UPANDAJI WA UFUTA
Shamba la ufuta ni budi likatuliwe na kulimwa vizuri kabla ya kupanda,hata hivyo pia unaweza kupanda bila kukatua lakini mavuno yatapungua kidogo.Inashauriwa kupanda ufuta kwa mistari kwa vipimo vifuatavyo.Sentimeta 50 kwa 10 au 50 kwa 20 kama utapanda kwa kutumia mistari ya kuchimba vijifereji vidogo katika mstari na kudondosha mbegu hizo katika vifereji hivyo (Drilling method) na kwa kuacha mche mmoja mmoja kwa kila shina.

Pia sentimeta 50 kwa 30 au 60 kwa 30 kwa kuacha miwili kwa kila shina. Kwa Mbegu ya Asili Unaweza Kupanda kwa sentimeta 70 kwa 30 kwa Kuacha Miwili kwa Kila shimo.Fukia mbegu kwa sentimenta .2.5 hadi 5.

MUDA WA KUPANDA
Muda mzuri wa kupanda ufuta ni mwanzoni mwa msimu wa kilimo yaani Mwishoni mwa mwezi Desemba hadi katikati kwa mwezi Januari.

MATUMIZI YA MBOLEA.... INAENDELEA BOFYA HAPA

 
Top