Taarifa  zilizopo  Tanzania  kutoka  FAO  zinakadiria  kwamba  mahindi  yanalimwa kiasi cha hekta milioni 4.12 za ardhi na kuzalisha tani milioni 5.36 za mahindi ya kula ambazo ni sawa na wastani wa tani 1.3 kwa hecta (FAOSTART,  2013).  Kwa  thamani,  mahindi  ni  zao  la  nne  kwa  umuhimu  kwa  mazao  ya  kilimo  yanayozalishwa  hapa  Tanzania  baada  ya  nyama  ya  ng’ombe,  ndizi  na  maharage  makavu.  

Katika  kuzalishwa  kwa  wingi,  mahindi ni zao la pili baada ya mihogo.
• Mahindi:  ni zao muhimu katika usalama wa chakula (na mbegu)
• Matumizi kwa chakula: ni gramu 308 kwa mtu mmoja kwa siku moja. Mahindi yanachangia wanga asilimia 61, protini  asilimia 50,  na ni asilimia 75 ya nafaka zote.
• Wazalishaji wakuu:  wakulima wadogo kwani huzalisha asilimia 85.
• Eneo:  Mahindi  ni  asilimia  45  ya  mazao  yote  yanayo  zaa  kwa  msimummoja na ni asilimia 60 ya nafaka za Tanzania.
• Kiuchumi:  mahindi  yanachangia  takriban  asilimia  20  ya  mapato  yoteyatokanayo  na  kilimo  katika  taifa  (GDP)  (NAP-Sera  ya  kilimo  ya  Taifa,2013).
 Uzalishaji kwa kanda  za ikolojia: Nyanda za juu kusini 46% ya mahindiyote - ~90% yanaenda kwenye ghala la Taifa,  kanda ya ziwa (17%),Kanda ya Kaskazini + kanda ya kati (14%), kanda za Kusini, Mashariki naMagharibi (23%).

Mahindi  yanastawi  vizuri  katika  kanda  zenye  mvua  ya  wastani  lakini kumekuwa  na  ongezeko  la  wakulima  wadogo  kulima  zao  hili  maeneo  yenye uzalishaji hafifu, maeneo yenye uhaba wa mvua na yenye uwezo hafifu  wa  uzalishaji.  Hali  hii  ni  tete  na  mkulima  anaweza  asivune  hata  kidogo kwenye maeneo hayo.

Hatari  ya  kupata  mavuno  kidogo  au  kukosa  mavuno  kabisa  inaweza  kurekebishwa kwa kutumia mikakati mbalimbali kama ifuatavyo:
•  Wakulima  katika  maeneo  makame  wanaweza  kushauriwa  kupanda mazao yanayostahimili ukame kama mtama;
• Mahindi yanaweza kupandwa kwa ufanisi zaidi iwapo wakulima wata-fuata  teknolojia  na  mbinu  sahihi  kama  kilimo  kwa  kufanya  matumizi  bora na uhifadhi wa  maji;
•  Matumizi  ya  mbegu  bora  zinazokomaa  mapema  na  zinazovumilia ukame;
• Kupanda kwa wakati;
• Kilimo hifadhi;
• Kufuatilia taarifa za utabiri wa hali ya hewa;
• Kupanda kwa nafasi sahihi;
• Njia sahihi za kuchanganya au kubadilishana mazao ya mahindi na mikunde kwa nafasi na nyakati tofauti;
• Matumizi ya mbolea za viwandani kwa kuzingatia S4 yaani zao sahihi, kiwango sahihi, kwa wakati sahihi, na kutumia njia sahihi pia  matumizi ya mbolea za asili kama mabaki ya mazao na samadi;
• Palizi ya uhakika na yenye tija;Njia  za  kupunguza  madhara  ya  wadudu  waharibifu  na  magonjwa,  pia  kuzingatia  S4. INAENDELEA BOFYA HAPA

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
 
Top