Kama ujawai kujiuliza, kujua zaidi au kufuatilia juu ya hili basi fuatilia kwa kina hili uweze kujua kiundani yaani Kama ni ajabu vile, jinsi umbo lako lilivyo limetokana na siku yako uliyozaliwa. Ili kujua hii njia inakupasa kujumlisha tarehe, mwezi na mwaka uliozaliwa ili upate tarakimu ya mwisho ya namba.
Jinsi ya kujua njia hii, kwa mfano umezaliwa 12.05.1990, unatakiwa ufanye hivi: 1 + 2 + 0 + 5 + 1 + 9 + 9 + 0 = 27 = 2 + 7 = 9.
Hii ina maana kwamba hiyo tarakimu ya mwisho ni tarakimu inayoelezea umbo la mwili wako ulivyo ambayo ni 9 katika mfano huu. Fanya hesabu hii ili uweze kujua namba yako na umbo lako binafsi; ukipata kati ya mojawapo ya namba hizi maana yake kama ifuatavyo:
Namba 1
Watu hawa wanakabiliwa sana na kitambi kutokana na ukweli kwamba metabolism yao inafanya kazi kwa kiasi kidogo sana na ipo chini sana.
Namba 2
Watu hawa wananyemelewa sana na kitambi ila mara nyingi watu hawa wanapendelea kufanya diet. Hata hivyo watu hawa wanakosea katika diet yao kwa kutojua chakula kipi hasa cha kula wakishikwa na njaa. Tahadhari kwa watu hawa inawapasa kutumia sana matunda, mboga za majani na mazoezi ya miili yao.
Namba 3
Watu hawa wana mtazamo wa kupenda sana mambo ya dunia na hii inachangia mzigo wa kiroho kuwaandama na kubadilisha uzito wao kwa ujumla.
Namba 4
Watu hawa wanashauriwa kujihusisha sana na mazoezi ya miili yao, kwa sababu ukosefu wa mazoezi kwa miili yao itawasababishia njaa na tamaa, ambayo kwa upande mwingine itasababisha mkusanyiko wa mafuta mwilini.
Namba 5
Watu hawa wanajua unene utayaharibu maumbo yao. Watu hawa wapo na maumbo madogo kiasi, wanapenda kuyafurahia maisha kwa kuzuia mkusanyiko wa mafuta katika miili yao.
Namba  6
Watu hawa wanachukuliwa kama watu wa bahati, wenye maumbo sawia, wanakula kwa kiasi na kwa kuyatunza vizuri maumbo yao.
Namba  7
Watu hawa kwa kawaida wanaongezeka uzito kutokana na masuala ya hisia, ambapo wakiweza kuwa na mahusiano mazuri na ya kudumu na wapenzi wao itawasaidia katika maisha yao.
Namba  8
Watu wa kundi hili wanashauriwa kujifunza kuacha mambo mengine yapite na kusamehe, kama wakiwa na hasira za mara kwa mara itachochea kuongeza mkusanyiko wa mafuta na kuongezeka kwa uzito.
Namba  9
Hatimaye, watu hawa wanakabiliwa na tishio la kitambi na ongezeko la mafuta. Kupunguza uzito kwa watu hawa mara nyingi inakuwa vigumu. Kuzuia ongezeko la mafuta kwa watu hawa ni jambo la muhimu na inawapasa watumie matunda yenye tindikali.


 
Top