Hebu leo tukae chini
tuangazie ni kwa jinsi gani unaweza kumtokea msichana mpya ambayw umekutana
naye kwa mara ya kwanza kabisa.
Lakini kama mwanamume,
jinsi ya kutongoza mwanamke ni jambo muhimu sana kujua tukiongelea suala la
mapenzi. Kile ambacho kinachohitaji kwanza kabisa ni kumfanya mwanamke
kama huyo akutambue yaani upate kufahamika kwake. Hii inakuwa rahisi kwa
kutumia mbinu hizi;
Mwangalie
Tuseme saa hizi uko na
marafiki zako ama uko peke yako katika sehemu ambayo ina watu wengi halafu huyo
mwanamke unataka kumtongoza yupo karibu na wewe ama sehemu mbali kidogo
na wewe.
Kile unachohitajika
sasa ni umuangalie ili ufanye kumuonesha kama unajaribu kumuangalia yeye.
Jaribu kujifanya unamuangalia kisirisiri, halafu akijaribu kukuangalia tu
unajifanya unashughuli nyingine ama unaongea na marafiki zako. Hii
itamsisimua kutaka kujua kwanini unamuangalia hivyo itamfanya na yeye
kukuangalia mara kwa mara kama utakuwa ukimwangalia.
Kila wakati
akikuangalia, wewe muangalie halafu papo hapo uangalie kando kikondoo. Endelea
kumuangalia kimtindo huo mara kwa mara na wakati mwingine, mwangalie nusu
sekunde, uangalie kando halafu hapo hapo muangalie tena, ukifanya hivyo utakuwa
unamsisimua kihisia. Lakini kama umejaribu njia hii yote halafu hakuonesha
dalili ya kuingiliana basi itakuwa hajakupenda ama kuridhika na wewe.
Jifanye kutoeleweka
Kama uko na marafiki
zako, muangalie mara kwa mara, lakini jifanye kama unasumbuliwa na jambo fulani
ambalo linakufanya wewe usielewe kile ambacho marafiki zako wanaongea. Hii
itamfanya yule mwanamke kufikiria kuwa ameingia kwa akili yako hivyo ataona ya
kuwa yeye ndiye chanzo kikuu kinachokuzuia wewe kumakinika na yale ambayo
marafiki zako wanaongea.
Mwonyeshe tabasamu
Bila kupoteza wakati,
hii itakuwa ufunguo wa kwako kufungua mlango wako wa kuongea naye kwani akili
yake yote itakuwa imekuja kwako hivyo lile unalohitajika la kufanya ni
kumwonyesha tabasamu. Fanya kutabasamu kiasi tu ili kuonyesha kuwa
wewe umevutiwa nae