Na Involatha  Beningnus - edonetz
Hayo ni baadhi ya mambo ambayo uwafanya mwanaume kupenda kuwa karibu sana na familia zao  kila wakati .Pia huwafanya wasitoke nje ya ndoa
na kufrahia familia zao zinapokua na Amani tele wakati wote
Kwa mujibu wa baadhi ya wanandoa wamedhibitisha haya
   HESHIMA;unachotakiwa kufanya ni kumsalimia mume wako uamkapo hata kwa kumkubatia au kumkiss ni ishara ya upendo , muulize unaendeleaje na baadhi ya maswali kuhusu afya take kwa unyenyekevu na upole .Muulize kuhusu siku mzima ratiba zake na anawaza nini siku hiyo ,kama una wazo jipya mshirikishe ,mfariji kwa maneno mazuri kama akikueleza jambo lake .

   UPENDO : Mpokee mumeo atokapo kazini mkaribishe kwa furaha, mtengee maji ya kuoga muoshe kama itawezekana ,mkande kwa ajiri ya kupunguza uchovu pia mpe chakula huku ukimsimulia kuhusu siku hiyo au hata stori nyingne za kufrahisha .

    USAFI : usafi ndio kila kitu kwa mwanamke, oga , nukia vizuri jipambe upambike wewe ni pambo ndani ya familia nunua mafuta mazuri ,nukia umvutie mumeo ,sio kunuka moshi , jifunze kwa khaki ya usafi ,mpaka mwanaume ajivunie kuwa na wewe . Panga vizuri nyumba yako angalau Mara 4 kwa wiki ili nyumbani kwako kuvutiwe kwa makazi .

     CHAKULA: Andaa chakula kitamu kwa ajili  ya mumeo nikiwa umevaa mavazi mazuri na masafi funga kitambaa kichwani kwa ajiri ya kutunza nywele zako zisiingie kwenye chakula .Pika chakula kwa umakini pia usichanganye vyakula sana ukapoteza maana , pika tofauti tofauti ili ale apendacho .
Ndoa yako itadumu kwa muda mrefu kama utafanya hayo, kila mwanaume ufurahia mapenzi ya kweli kutoka kwa mke, mpenzi au mchumba na kumpelea kutamani kuwa nae kila wakati .
mtu mkubwa usikae mbali nami nitakujuza kila yanayostahili usikose kufuatilia kupitia facebook,inst na twiter kote ni @edonetz karibuni wote. ahsante
 
Top