kuna mambo mwanaume unaweza kuyachukulia kimzaa mzaa hila hakika penzi litakua na kukua kila iitwapo leo endapo utazingatia suala hili kwa ukaribu na kiundani zaidi unatakiwa kulijua na kuliweka katika ratiba zako za kila siku
iko hivi  Mwanasaikolojia na Mwalimu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam maarufu kama Chriss Mauki ambaye ameongelea swala la mawasiliano kuwa moja ya vitu ambavyo wanawake wanapenda ingawa wanaume wengi wanashindwa kutekeleza hilo swala kwa kuona halina umuhimu. Yaani wanawake wanapenda mawasiliano wanapenda uwasiliane wajue uko wapi unafanya nini na nani, wanaume wengi wakishaulizwa maswali kama haya wanakuwa wakali, kuna mahitaji ambayo wote wanafanana na kuna vile wanavyovipenda kama kuambiwa ukweli lakini mwingine anakataa mimi bora asiniambie kitu chochote.
Wanawake wanapenda ukaribu kujali hisia zake, kuzungumza nae kuonesha una mjali, kuonesha unamuamini na kumpa kipaumbele katika maisha ya kawaida hata kwenye mahusiano, vile vile mwanamke anapenda kujaliwa katika matatizo na kusifiwa pale  anapofanya kitu sahihi hii pia ni katika maisha ya mapenzi na hata nje ya mapenzi. Katika mahusiano mwanamke anapenda kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake kiafya, kihisia na kiuchumi pia mazungumzo ni muhimu kwa sababu mwanamke huumizwa sana na vipindi virefu vya ukimya sio tu kwamba wanataka mazungumzo bali mazungumzo yenye kuleta hamasa katika maisha na yenye mvuto ndani yake.

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW

FACEBOOK@EDONETZ  ,TWITER@EDONETZ INSTAGRAM@EDONETZ NA YOUTUBE@EDONETZ TV
 
Top