Kitambi  ni  ile  hali  ya  tumbo  kuwa kubwa  na  kuchomoza  kwa  mbele  na wakati mwingine  kufikia  hatua  ya  kunin’ginia.
 AINA KUU 6 ZA VITAMBI.
 1. KITAMBI MVURUGO - Hiki kitambi kimekaa kama O
kinapatikana kwa kula sana kitimoto
 2. KITAMBI MCHUCHUMIO - Hiki kitambi kimekaa kama herufi D kinatokana na kula sana michemsho na bia za ofa
3. KITAMBI MBONYEO - Akivua shati kitovu hakionekani. Hiki wanacho wala rushwa, ila akisimamishwa kazi kinaisha haraka sana.
4. KITAMBI MTEPETO - Ni kitambi cha wastani ambacho ukivaa nguo pana hakionekani. Hiki kinasababishwa na kula mno vipolo
5. KITAMBI MFUMANIO - Hiki mtu anakuwa hana pesa ila kitambi ni kutokana na minyoo na utapiamlo wa ukubwani
6. KITAMBI MTUNGUO - Hiki wanacho sana akina dada na wanawake, kina umbo la yai. Hiki kwa "diet" hakitoki labda kwa maombi tu. Share na washikaji zako.
JINSI  KITAMBI  KINAVYO  PATIKANA
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, mwili wa binadamu una seli kati  ya bilioni 50  hadi 200 za mafuta zilizogawanyika katika  sehemu mbalimbali  za  mwili wa binadamu.
Kwa wanawake  seli hizo  zipo sana katika maeneo ya matiti, kwenye  nyonga, kiunoni na kwenye makalio.
Kwa upande  wa  wanaume seli  hizo zinapatikana  sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio pia.
Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili:
i.   Njia  ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi
ii.  Na  njia  ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo, kongosho n.k
SABABU ZA KUPATA KITAMBI
Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu(kalori) katika  mwili wa  mwanadamu, hali  inayo  sababishwa  na  mtu  kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.
Vyakula vinavyochangia  kuleta  kitambi ni  pamoja  na :
i.  Vyakula  vyenye  mafuta  mengi  kama  vile  nyama nyekundu  (iwe ni ya kuchemsha, kukaanga au kuchoma), nyama  ya  kuku  wa  kizungu  ( iwe  ya kuchemsha, kukaanga  ama  kuchoma ), mafuta ya kupikia, (hasa yale yatokanayo na bidhaa za wanyama, kama siagi, na jibini), viazi ya kukaanga kwa mafuta  (chips) pamoja  na  pizza.
ii. Vyakula vyenye wanga mwingi kama  vile ugali wa mahindi, mihogo, wali, mkate  mweupe.
iii.  Vyakula  na  vinywaji  vyenye  sukari  nyingi  iliyo  ongezwa
kama  vile  soda  na  keki.
iv. Vyakula  vilivyo  tengenezwa  kwa  ngano  na  sukari kama  vile  keki, skonzi, chapatti, maandazi, mkate  mweupe  nk
v. Pamoja  na  vinywaji  vilivyo  tengenezwa  kwa  kutumia  ngano  kama vile  bia  za  aina  mbalimbali  na  nk
Vyakula  vilivyo  tajwa  hapo  juu, vikitumiwa  bila  kuzingatia  kanuni  za  mlo kamili, huchangia  kuleta  tatizo  la  kitambi.
vi.Sababu nyingine ni  kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na  viungo
kwa  muda  mrefu.
JINSI YA KUJUA KAMA UNA KITAMBI
Kitambi kinaweza kuonekana kirahisi kwa macho. Ila kujua ni kwa kiwango gani kitambi chako kipo inabidi kufanya vipimo vya kiuno na nyonga
Mzingo wa kiuno ukiwa >102 cm au 40  kwa wanaume na >88 cm au 35  kwa wanawake, na uwiano wa kiuno na hips(Waist-Hip Ratio) ikiwa >0.9 kwa wanaume na >0.85 kwa wanawake.
BMI ya 30 au zaidi inaashiria ‘Obese’ uzito kuzidi kiasi. Kuwa na mzingo uliozidi kawaida ni kiashiria hatari cha matatizo ya kimetaboliki, kuliko hata cha BMI.
Kipimo kingine cha kitambi ambacho kimeonyesha uwezo zaidi kuliko BMI katika kutabiri uwezekano mkubwa wa magonjwa ya moyo ni Index Of Central Obesity(Waist-To-Height Ratio-WHtR) ambapo uwiano ukiwa sawa na 0.5 au zaidi, hii ikimaanisha mzingo wa kiuno angalau ni nusu ya kimo cha mtu.
Kipimo kingine ni Body Volume Index, kinachopima kitambi kwa kupima umbo la mtu na mgawanyo wa uzito wake.
MAMBO  YANAYO  MUWEKA  MTU  KATIKA  HATARI  YA KUPATWA  NA  KITAMBI
Tumekwisha  ona  hapo  juu jinsi  kitambi  kinavyo  patikana  na  vyakula pamoja  na  sababu  nyinginezo  zinazo  sababisha  kutokea  kwa  kitambi, sasa tutazame  mambo  yatakayo  kufanya  uwe  katika  hatari  ya  kupatwa  na kitambi.
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za kitaalamu, mambo  yafuatayo  huwaweka watu  katika  hatari  kubwa   ya  kupatwa  na  kitambi :
1.Ulaji  mbovu  wa  chakula; Ulaji  mbovu  wa  chakula  ni  ulaji  usio zingatia  kanuni  za  mlo  kamili. Hapa  mtu  hufululiza  kutumia  chakula  cha aina  fulani  pekee  bila  kuzingatia  aina  nyinginezo  za  chakula.  Mfano; mtu anaweza  kuwa  anakula  mlo  ufuatao :
Asubuhi :  Mchemsho  ama    supu  ya  ng’ombe , chapatti  tatu  na  soda moja. Mchana :   Ugali  nyama  choma anashushia  kwa  maji  na  soda.
Jioni :  Mchemsho  wa  kuku  na  bia  mbili  nakuendelea.
Usiku  :  Chips  mayai  au  chips  kuku  au  chips  mishikaki  na  bia.
Mtu  huyu  akiendelea  na  utaratibu  huu  kwa  muda  mrefu, ni  lazima atapatwa  na  kitambi.
2.  Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  mafuta  mengi
3.  Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye wanga  mwingi  .
4. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  sukari  iliyo  ongezwa
5. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vya  ngano.
6. Ulaji  mfululizo  wa   vinywaji  vyenye ngano  na  sukari.
7. Kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na viungo 
Mhusika  anapokuwa  katika  makundi  yote  yali yotajwa  hapo  juu, hali  huwa mbaya  zaidi.
NJIA ZA KUONDOA KITAMBI
Kuwa  na  kitambi  ni  lugha  ya  mwili  ( body-language )  inayo  leta  ujumbe kwako  kwamba  “ Mwili    wako  haupo  salama  tena
Kama  una  kitambi   maana  yake  una  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini, mwili wako  unatumika  kuhifadhi  mafuta  usiyo  yahitaji.
Hali  hii  kitabibu  imaanisha  kwamba, ogani  nyinginezo  zilizomo  ndani  ya mwili  wako  zinao gelea  kwenye  mafuta yasihotajika  yaliyomo ndani  ya mwili  wako,  jambo  linalo  kuweka  katika  hatari  kubwa  sana  ya kushambuliwa  na  magonjwa  hatari  kama  vile  shinikizo  kubwa  la  damu, kiharusi  na kisukari  na  kwa kutaja  machache.
Hivyo  basi  ili  kuondokana  na  hatari  hiyo, yakupasa   kupambana  kuondoa hayo  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini  mwako.
NJIA  ZA  KUONDOA  KITAMBI.
Unaweza  kuondokana  na  kitambi  kwa  kufanya  diet  pamoja  na  mazoezi ya mwili  na  viungo.
Vilevile  unaweza  kuondoa  kitambi  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa kutumia  dawa  asilia  ya  kuondoa  kitambi  na  kuondoa  mafuta  yasiyo hitajika  mwilini.
Mi naona sanasana ni vizuri kufanya mazoezi ili kuondokana na kitambi au kupata ushauri wa dakitari moja kwa moja

Unaweza kushea www.edonetz.blogspot.com
 
Top