China ni nchi ambayo inazidisha  matumizi yake ya vioo kuunda vivutio vya kitalii kwa kujenga choo cha vioo ambacho mtu anaweza akaona nje na hata ndani.
Vyoo hivyo, vimejengwa karibu na
Ziwa Shiyan, katika mkoa wa Hunan kusini mwa nchi hiyo.
Vioo hivyo vinawezesha wanaovitumia vyoo hivyo kutazama mandhari ya kuvutia ya msitu au wengine wanaotumia vyoo jirani.
Aidha, walio nje wanaweza kuona walio ndani ya vyoo.
Kuta za vyoo hivyo, hata zile zinazotenganisha vyoo vya wanawake na wanaume, ni za vioo kabisa ingawa vioo hivyo vimetiwa ukungu kiasi na Vyombo vya habari nchini humo vinasema ni watu wachache sana waliotumia vyoo hivyo siku ya kuzinduliwa kwake.
Licha ya umaarufu wa mijengo ya kutumia vioo katika ujenzi, hasa kwenye madaraja na barabara, baadhi ya miradi imefungwa.
Habari za kuzinduliwa kwa vyoo hivyo zimevuma sana.hasa mitandaoni ambapo wtu mbalimbali wametoa maoni tofauti tofauti juu ya hili.
Ejike Nnadi, alichangia katika ujumbe wa Facebook wa runinga ya taifa CCTV amesema: "Hapana".
 Ingawa  kunao wengine wanaosema wanaweza kujaribu kuvitumia.
Tina Chen anasema mradi huo wa vyoo ni ishara kwamba kuna mtu alikuwa na pesa za "kupoteza".

Mi nirudi kwako mtu mkubwa msomaji wangu unaweza kuvitumia vyoo hivyo vikija hapa bongo?
 
Top