Na Involatha benignus wa edonetz
Zawadi pekee ya mzazi kwa mototo ni malezi bora ambayo yata mpeleka popote na kufanya chochote kwa muda muda anaotakiwa ukimuuliza mtu ambaye amefanikiwa kwa kitu Fulani siri ya mafanikio yake atakwambia ni malezi ya wazazi na nguvu ya mungu,
swali wewe unamleaje mototo wako, katika mazingira gani,na kwa njia gani, na tambua kuwa Kawaida ya mtoto ufuata tabia inayomzunguka iwe ni kwenye familia,shule,au mazingira ya karibu haijarishi ni mbaya au nzuri. Soma njia hizi zitakusaidia sana…..
1.Maadili ya dini
Ni vyema mtoto umfundishe kuwa hofu ya Mungu ,tunajua kanisani au msikikitini ni sehem nzuri ya malezi , mfundishe mtoto kuongea vizuri na watu pia kua na hekima au busra wewe mzazi/ mlezi usitoe maneno yasiyopasa mbele za mtoto, mfundishe kutofautisha nyakati hapa nipo na mkubwa  ,baba, mama, mlezi, babu, bibi, Dada, kaka, nk, atofautishe maongezi ya mkubwa na mtoto mwenzie .

2) Mfundishe mtoto jinsi ya kuvua samaki na siyo kumpa samaki 
Anza kumjengea tabia nzuri mtoto angali akiwa mdogo mpe njia za kufanikiwa, wewe kama mzazi umepitia mengi hivyo basi kupitia makosa yako umejifunza mengi sana kwa hiyo mfundishe mtoto apite njia nzuri ili asije kurudia makosa kama yako ,mfundishe mabadiliko ya yanayoendelea duniani ili ajiandae na mabadiliko hayo. Usimlee tena katika mfumo wetu wa elimu ambapo unaandaliwa kuwa mwajiriwa, mlee katika mawazo ya kujitegemea, kujiajiri, jinsi ya kuona fursa katika jamii na kuzitendea kazi, jinsi ya kutengeneza ajira na siyo kuajiriwa tu kwani kazi za maofisini siku hizi zimekuwa changamoto hivyo basi ni vema kumwandaa mwanao katika mabadiliko haya ambayo yapo na yataendelea kuwepo. 
3 UPENDO
mfundishe upendo mwanao, tambua kua upendo ndio kitu muhim sana kwa malezi pia ni muhim ndani ya familia na pia taifa.UPENDO huepusha mambo mabaya kama,matusi,Ugomvi,wizi, na vitendo vyoa kigaidi.Wapo  baadhi ya wazazi ambao hawatambui kabisa nini maana ya upendo uwafundisha matabaka watoto wao  hawatambui kua mtoto unaweza akasambalatisha familia kwa siku moja kwa chuki unapompadikizia kila siku, kwa sababu ya chuki ndo maana vita haviishi kwa baadhi ya kabila na nchi, ila  wazazi wakitambua hilo Leo lazima  vita vitaisha duniani .
4) Usimnyime mtoto adhabu anapokosea 
Mtoto ana haki ya kuadhibiwa pale pale tu anapofanya makosa ambayo anastahili kuadhibiwa. Sasa kuna wazazi wengine wanalea mtoto kama yai mtoto anageuka mfalme ndani ya nyumba au mtawala, mzazi hana kauli mtoto anafanya chochote anachojisikia ndani ya nyumba kama vile kuvunja vitu na kuharibu bila hata kumpa adhabu ili akome tabia hiyo. Mtoto anatukatana watu, na wakati wengine wazazi nao huwa wanatukanwa na watoto wao yote haya ni kwa sababu ya kukosa malezi bora, unamnyima adhabu ndio matokeo yake tabia inakuwa na mtoto umleavyo ndivyo akuavyo na samaki mkunje angali mbichi. 
Kwa hiyo, mtoto kuwa na kutokuwa na heshima chanzo ni mzazi umeridhika na hali hiyo ambayo mtoto wako anayo bila kuchukua hatua. 

5...Elimu 
zawadi kuu katika maisha mototo hadi ukubwani  atakukumbuka milele kama elimu ,Elimu ni ufunguo wa maisha , tambua kua mtoto ukimfundisha au ukimpa elimu ataweza kutambua baya na zuri haijarishi ni Elimu ya darasani,au ya maisha (stadi za maisha)
Mtoto ukimpeleka shule kusoma akishakuwa na maadili ya dini , hofu ya Mungu, adabu pia na utii, atawasikiliza mwalimu wake na kufaulu masomo yake. Elimu ya darasani ni muhim kwa mtoto kwa sababu itampatia kipato na kuacha mawazo mabaya au tamaa ambazo zinaweza kumshawishi kutenda mabaya. Hata Elimu ya Dunia
Mfundishe mtoto kujitambua kua yeye ni nani pia changamoto anazoweza kukabiliana Nazi kimaisha , shuleni, mtaani na kifikira ili atambue mapema sio baada ya kukabiliana Nazi ndo unamfundisha , utakua umemyima haki zake za msingi .

6) Mfundishe mtoto kukosa 
Maisha ya binadamu ni mafupi kwa hiyo huwezi kukaa na mwanao siku zote inakupasa kumfundisha mtoto kukosa pia wakati mwingine ni vizuri sana mfano mtoto anataka kitu fulani analia ameshasoma saikolojia yako mzazi, wewe ukiona tu mtoto analia unamtimizia hata kama kitu siyo cha maana anampa tu hata kama una hela muda mwingine mwambie sina ili ajifunze kukosa mpe hata siku nyingine ,waingereza wanasema hivi’’ teach your child to learn or to face disappointment’’ maana yake tuwafundishe watoto kukosa au kukutana na changamoto ili wajifunze.
 

7.Uwajibikaji
Mbali na elimu mfundishe mtoto kuwajibika kwa namna moja au nyingine mfano kazi za nyumbani ,kazi ndogo ndogo kulingana na umri wake mwambie maneno ya busara na ya kumfariji pindi anapokua anawajibika, pia ndani ya uwajibikaji mfundishe Matumizi ya pesa
Ili atambue mapema kua hakuna kazi ya kawaida kila kazi inaitaji moyo na akili na kupata pesa lazima upambane .

8 .Maendeleo
Usimpe mtoto pesa ya kuchezea anaweza  kutumia pesa hiyo vibaya ukihisi unamlea vizuri kumbe unampteza , mpe  mtoto pesa kwa malengo pia usimbanie mtoto au kumyima mtoto pesa ila  akueleze  niya matumizi gani pia mfatilie uone nini faida ya pesa hile na ameitumia kwa lipi.
Mfundishe mtoto kwa vitendo ,Pima uelewa wake na kumbuka  kua ukiwa mzembe wa kufikiri na mtoto anakuwa vile vile ukiwa na maendeleo na mtoto anatamani awe na maendeleo kama yako , baadhi ya watoto hupenda kusema nataka niwe doctor kama baba au mama. Hapo ndo unatambua  kua mtoto kuishi kwa kupenda kile kinachomzunguka..
9. Mwisho, wape watoto chakula bora ambavyo vitawapa afya bora ya mwili na kinga dhidi ya magonjwa na hapa nazungumzia vyakula vya asili na siyo vya viwandani kama vile matunda, mboga za majani na siyo soda, pipi biskuti nk. Mpe mtoto ratiba ya kusoma vitabu au mambo yake ya darasani na siyo kuangalia tv kwa muda mrefu.

Hitimisho 
Hizo ni baadhi ya misingi ya malezi ya mtoto ambayo ni rahisi kwa kila mzazi kumlea mwanae kwa njia inayofaa  " fuata nyuki ule asali " baadhi ya wazazi wanaofuata hizo mbinu tunaona mafanikio cha msingi mzazi /mlezi   hakuna kusubiri Anza sasa ,watoto wengi wamekosa misingi hiyo wapo mtaani bila kazi, na kujiingiza katika makundi mabaya kama mateja,magaidi nk  Fanya hivo usaidie kutokomeza umasikini Tanzania  na ugaidi.
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW

FACEBOOK@EDONETZ  ,TWITER@EDONETZ INSTAGRAM@EDONETZ_blog NA YOUTUBE@EDONE TV
 
Top