Hakuna kitu kinacholeta mkangamyiko katika ndoa kama migogoro ya mawifi yaani ndugu wa mume hadi wengine utakuta wanarushiana maneno makali bila sababu za msingi ingawa sio wote hila walio wengi wako vile na Maisha ya ndoa ni matamu sana ikiwa mume na mke wataishi kwa amani na upendo, kubwa hao mawifi hujiona wana haki zaidi kuliko mwanamke huyo kwa sababu  mumewe ni ndugu yao wa damu, lisikupe shida hili fanya yafuatayo.
TUMIA BUSARA  KATIKA MAAMUZI
Lazima uwe na busara na moyo wa uvumilivu ili uweze kukabiliana na mawifi wakorofi. Mwingine anaweza akawa analala kutwa nzima bila kusaidia kazi za nyumbani halafu mume anapokuja jioni anakuwa wa kwanza kumwambia maneno ya ajabu, Hata kama amemwambia kaka yake kuwa labda hushindi nyumbani, baada ya yeye kuondoka asubuhi na maneno mengine mengi kutokana na chuki zake binafsi, unapaswa kutumia busara za hali ya juu. tumia lugha nzuri ni wazi kuwa mumeo atakuelewa na kukusamehe ambapo naamini kuwa usiku huo utakuwa wenye kila aina ya furaha na bashasha zilizojaa  cheche za mapenzi.
MTAMBUE TOKEA MWANZO ALIKUWAJE?
Jinsi unavyoanza ndivyo unavyomaliza, kama ukivurunda kitu kuanzia mwanzo, tarajia kuharibu mpaka mwisho. Kinachotokea mwishoni ni kupunguza madhara ya tatizo ambalo tayari limeshatokea na lina madhara makubwa, Inawezekana tangu ulipokwenda kijijini kwao (ukweni) ulishaona baadhi ya tabia zake mbaya ambazo kwa namna moja ama nyingine zilikukwaza.
Kwanza mumeo atakapokupa taarifa ya ujio wa wifi yako, usioneshe kukasirika, kwa sababu kama ukionesha umekasirika, anaweza akahisi jambo fulani baya kwako, Pengine atahisi humpendi dada yake hivyo hata siku akikukosea na kumwambia ataamini ni fitina au chuki zako binafsi. Siku wifi yako anapokuja nyumbani, kuwa wa kwanza kumkumbusha mumeo kwenda kumpokea kituoni, weka maandalizi motomoto na onyesha furaha ya ujio wake.
MALIZENI WENYEWE KWA MAZUNGUMZO
Ikiwa wifi yako amekukosea jaribu kuzungumza naye. Inawezekana ghafla alianza kuwa na maneno ya hapa na pale au wivu usioeleweka, pengine alimwambia mumeo, kuwa una tabia mbaya au vyovyote katika kukuharibia ndoa yako. Usionyeshe chuki, zungumza naye taratibu, Mueleze jinsi unavyompenda na kuuthamini uhusiano wenu. Ikiwa utatumia lugha nzuri naamini atakuelewa lakini kama siyo muelewa ataendelea na chokochoko zitakazokukera.
MSHIRIKISHE MUMEO
Kama yote hapo juu hayakufua dafu, unapaswa kukaa chini na mumeo na kumweleza juu ya jambo hili. Kukaa kwako kimya na kumvumilia kutakuwa hakuna maana, kwa sababu ni rahisi ndoa yako kuvunjika, Usimfiche chochote, hata kama aliwahi kukutolea maneno machafu kwa mumeo, usijali, zungumza taratibu bila jazba huku ukitumia hoja kuliko maneno matupu!!!!!
Nyumba ni kwa ajili yako na mumeo. Kuolewa hakumaanishi kwamba umeolewa na ukoo mzima na kila mmoja anaweza kukudhihaki na kukutukana, Lazima utambue haki yako na kama mumeo ana mapenzi ya dhati kwako, lazima atakupa kipaumbele na kufanya maamuzi sahihi kwa heshima na sababu ya kuilinda ndoa yenu ambayo ni muhimu sana.
JIUNGE NASI
FB@EDONETZ TWITER@EDONETZ INST@EDONETZ_BLOG YOUTUBE@EDONE TV


 
Top