karibu sana katika story kubwa kwa siku ya leo zote kaliiiii!!!!!!!!!!!!!!


Msami et Barakah da Prince hana nguvu ya kuwa mume wa Naj
Msanii wa muziki na mwalimu wa dance, Msami Giovani anayefanya vizuri na wimbo wake ‘Step by Step’ amesema Barakah The Prince bado hana nguvu ya kuwa mume wala kuwa mchumba wa Najma.
Ametoa kauli hiyo baada ya Barakah kumtukana Msami baada ya kukoment katika akaunti ya Instagram ya Naj.
Akiongea na E-News ya EATV, Msami alisema, “Kwanza Barakah ajue Naj sio mke wake, wala mchumba wake ni boyfriend na girlfriend tu. Kwahiyo Barakah hana nguvu ya mume wala mchumba kwa Naj. Kwahiyo hata mtu mwingine anaweza kuleta fujo na kutupa kete yake. Halafu mie ni expensive sana kwa Naj watu ambao naweza kurusha kete yangu kwa watu ambao ni expensive ambao wapo kwenye level yangu kama mimi. Naj yupo kwenye level ya Barakah na mimi nipo kwenye level nyingine kabisa za juu. We angalia watu wangu awe Uwoya au Kajala, kwahiyo mimi ni expensive sana.”

AliKiba na Mr Blue waungana kumrudisha Abby Skills
Msanii ambaye alifanya vizuri kipindi cha nyuma na nyimbo ‘Maria’ na ‘Mimi na Wewe’ Abby Skills anajipanga kurudi upya katika game la muziki na wimbo ‘Averina’ akiwa na Ali Kiba.

Muimbaji huyo amesemaa kuwa AliKiba na Mr Blue ndiyo watu ambao wanamsimia kwa sasa ili kumrudisha upya kwenye chati.
“AliKiba na Mr Blue walikaa chini na kuamua kunisaidia kunirudisha kwenye game,” alisema Abby. “Waliniambia tumeona una kipaji kizuri, una melody ngoja tushirikiane ili kukupeleke sehemu fulani,”
Aliongeza, “Hata hii project yangu mpya na AliKiba ‘Averina’ wao ndio wanasimamia kila kitu, kwa hiyo kuna mambo mazuri yanakuja hivi karibuni,”
Muimbaji huyo amesema kazi yake mpya aliyomshirikisha AliKiba itatoka hivi karibuni kwa kuwa tayari ameshashoot na video.

Ukimya wa muda mrefu Ray C’ Chalamila’ uko mbioni kuzimwa kwa kishindo
Ukimya wa muda mrefu wa Rehema ‘Ray C’ Chalamila’ uko mbioni kuzimwa kwa kishindo. Ni kwasababu mwanamuziki huyo mkongwe, ameingia studio za Wanene Entertaiment jijini Dar kurekodi kazi mpya. 
Muimbaji huyo ambaye kwa muda mrefu amekuwa akipambana na uraibu wa madawa ya kulevya, amepata mshirika mjuzi wa kumuongoza katika mrejeo wa nguvu – Damian Soul.
all the best ray c

Mr Nice  kwanini anakubalika Kenya?
Mwanamuziki, Lucas Mkenda ‘Mr Nice’ amesema ukongwe wake kwenye muziki ndiyo kitu ambao kinampatia mashavu zaidi nchini Kenya.
Alhamisi hii, Mr Nice amesema Kenya ni sehemu pekee ambazo anaweza kufanya show nyingi bila mashabiki kumchoka.
“Najivunia kuwa rafiki namba moja wa Wakenya,” alisema Mr Nice. “Hiyo ni silaa yangu kubwa katika muziki wangu, kwa hiyo labda ni kwa sababu tayari tumeshatengeneza chemistry nao toka naanza kufanya muziki,”
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na albamu yake ya Kioo, hivi karibuni alijaza umati wa mkubwa katika show yake iliyofanyika katika club moja huko nchini Kenya.
Muimbaji huyo ijumaa hii atakuwa mjini Kisumu na Jumamosi atakuwa katika jiji la Nairobi maeneo ya Embakassy katika muendelezo wa show zake. 
mashabiki wa Afrika Kusini wanahamu na Raymond kwenye MTV MAMA 2016
Jumamosi hii ya Oktoba 22, mwaka huu zinatarajiwa kufanyika tuzo za MTV MAMA 2016 kwenye ukumbi wa Ticket Pro Dome, Johannesburg, Afrika Kusini lakini imedaiwa kuwa Raymond ameonekana kuvutia zaidi kwenye tuzo hizo.
Mtangazaji anayefanya vizuri kwa sasa kupitia Times FM na kipindi chake cha The Playlist, Omari Tambwe aka Lil Ommy ambaye ameweka kambi nchini humo kwa ajili ya kushuhudia tuzo hizo amesema kuwa mashabiki wamekuwa wakiwasubiri wasanii wengi lakini shauku yao kubwa ipo kwa Raymond wa WCB.
“Wanasubiriwa wasanii wengi lakini, shauku zaidi ipo kwa Raymond watu wengi hapa wameanza kumfuatilia, wengine wakiwa na hamu ya kumshuhudia kuzingatia ni msanii mpya halafu kipengele chenyewe kina uzito yaani msanii aliyeingia na kufanya vizuri,” Lil Ommy ameiambia Times FM.
Raymond anawani kipengele cha msanii bora anayechipukia, wao wanakiita Best Breakthrough Act akiwa na wasanii wengine kama Simi (Nigeria), Nathi (Afrika Kusini), Nasty C (Afrika Kusini), Franko (Cameroon), Falz (Nigeria) na Emtee (Afrika Kusini).


Feza Kessy anahisi Nando anadata 
Staa aliyewahi kuiwakilisha Tanzania katika shindano la Big Brother Africa, Feza Kessy, amesema kuwa anaamini Nando aliyewahi kushiriki naye kwenye shindano hilo, amepatwa na tatizo au anaugua kwakuwa tabia anazozionyesha zinampa mashaka.
Akiongea kwenye kipindi cha Kubamba kupitia Times FM, Feza amesema anaona akili ya Nando kama imevurugika kwa sasa. Anasema amekuwa tofauti na Nando, yule kijana mwenye nidhamu na mpole aliyekuwa akimfahamu.
“Naamini Nando ana tatizo asaidiwe,” alisema Feza. “Sijui kwanini lakini naamini Nando ana something hayupo sawa, sio yule Nando ninayemfahamu, naomba atafutwe asaidiwe,” alisisitiza.
Feza ambaye kwa sasa ni mtangazaji wa Choice FM, amedai kuwa aliwahi kukutana na Nando na akampa noti ya shilingi elfu 10. Anasema badala yake yake staa huyo aliitupa chini kwa madai kuwa haiwezi kumsaidia kitu.

 ..................................................................
Vanessa Mdee amezidi kutanua jina lake nchini Nigeria. Wimbo alioshirikishwa na rapper wa Nigeria, Ice Prince ‘No Mind Dem’ umefanikiwa kuwa moja kati ya nyimbo zitakazopatikana kwenye albamu mpya ya rapper huyo ‘ ‘Jos To The World’.
Ice Prince anatarajia kuachia albamu yake hiyo ya tatu Oktoba 28, mwaka huu baada ya ile ya ‘Everybody Loves Ice Prince’ na ‘Fire of Zamani’ ambayo itakuwa na nyimbo 18.
Ndani ya albamu hiyo amewashirikisha wasanii wengine kama Phyno, Tiwa Savage, Run Town, Yemi Alade, Dj Buckz na wengine.

Mwanamuziki nguli wa Kenya Achieng Abura afariki dunia
Mwanamuziki mkongwe wa nchini Kenya na aliyewahi kuwa Principal kwenye mashindano ya Tusker Project Fame, Achieng Abura amefariki dunia.
Kwa mujibu wa The Standard, amefariki Alhamis hii kwenye hospitali ya taifa ya Kenyatta jijini Nairobi. Bi. Abura alikuwa amelazwa katika wodi binafsi akitibiwa ugonjwa ambao haujajulikana.
Bi. Abura Alifariki dunia mida ya saa 12 jioni. Mapema mwezi huu, muimbaji huyo aliandika kuwa afya yake si nzuri na madaktari walimshauri aongeze uzito kisha kuupunguza kupitia mazoezi.
Chanzo cha karibu na familia yake kilidai kuwa alihamishwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi baada ya hali yake kuwa mbaya.
Wasanii mbalimbali wa Kenya wametuma salamu zao za rambirambi kupitia mitandao ya kijamii. Hawa ni baadhi yao.
Avril
My day ends on a sad note..don’t know what to say…RIP Achieng Abura :'( ..
Nameless
So sad to hear of your passing dear sister….Rest in peace Achieng Abura.
Akothee
You’ve done your part….it’s a journey…I mourn you ! RIP #RIPAchiengAbura
Sauti Sol
Our heartfelt condolences to the family and friends of the late Achieng Abura. She was a natural talent, mentor to us all. This is a big blow to the music industry! #Rip #RipAchiengAbura #Shujaa
The King Kaka
Rest In Peace.
Achieng Abura.
Safiri Salama, tutaonana Baadaye.
Amani

R.I.P. Achieng Abura 
…a lovely woman who was passionate about music #legend
 
Top