KILA kitu uwaga kina kazi mwilini katika mfurulizo wa makala hizi leo tuangazie ganda la chungwa ila ukizingatia itakusaidia sana fuata utaratibu vizuri ,Watu wengi husumbuliwa na ugonjwa wa mba kichwani na mara nyingi mba huwatokea nyakati za baridi kwani kichwa huwa ni kikavu sana; kama unasumbuliwa na hilo tatizo unatakiwa kuwa makini na mafuta unayotumia na kuhakikisha unatumia mafuta kila unapoosha nywele zako.
FANYA HIVI!!!
Chukua chungwa limenye upate maganda yake baada ya hapo chukua limao likamue kisha uweke kwenye brenda usage upate mchanganyiko mmoja.
NA KWA UPANDE WA MATUMIZI
Osha nywele zako kwanza zitakate na baada ya hapo zikaushe kisha paka mchanganyiko wako kwenye ngozi acha kwa muda wa dakika 20-25 kisha osha kwa kutumia shampuu unayotumia ambayo unaamini ni nzuri.

Tumia tiba hii kwa wiki mara tatu utaona jinsi utakavyokomesha moja kwa moja tatizo la mba kichwani.ukiona tatizo limezidi pata ushauri wa daktari…

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top