Kutoa huduma ya kwanza ni mhimu sana kwa binadamu wa kawaida na kutoa huduma ya kwanza sio kitu kigeni kwa walio wengi wanaelewa vizuri tu na  Watu wengi sasa wana ujuzi wa huduma ya kwanza, wakikutana na hali ya dharura huwa hawahangaiki kama zamani. Lakini njia zisizo sahihi wanazotumiwa zinaweza kuharibu miili yao. Yafuatayo ni makosa wanayoweza kufanywa wakati wa kutoa huduma ya kwanza, hivyo kama mtoa huduma unapaswa kuyaepuka.
1.Kuinua kichwa wakati pua ikitokwa na damu, 
wataalamu wa masuala ya afya wanaeleza kufanya hivyo kunaweza kusababisha damu kutiririka na kuingia kwenye koo na kusababisha ukosefu wa hewa. Inashauriwa endapo utatokwa na damu puani baada ya kujeruhiwa, usitumie vitu vyovyote puani kuzuia damu hiyo kutoka, kwani ukifanya hivyo inawezekana ukasababisha ubongo wako kuambukizwa na virusi.
2. Usitumie dawa ya meno unapoungua, 
watu wengi wakiungua, wanapendelea kutumia dawa ya meno kupunguza maumivu, hii ni hatari sana tena usijaribu kabisa kuweka dawa ya meno juu ya sehemu uliyoungua kwani endapo utafanya hivyo unaweza kusababisha mahali palipoungua kuambukizwa na virusi. Njia sahihi inayoshauriwa kufanyika ili kushughulikia tatizo lililojitokeza ni kutumia maji baridi kusafisha na kupunguza digrii ya joto sehemu iliyoungua.
3.Usimwinue kwa haraka mzee aliyeanguka, 
kusaidia wazee walioanguka kusimama mara moja ni hatari sana, wanasayansi wanasema mifupa ya wazee wengi huvunjika kirahisi na huchukua muda pia hadi kujiunga na kurudi katika hali yake ya kawaida. Endapo utahitaji kutoa huduma ya kwanza kwa mzee aliyeanguka unashauriwa usimfanye asimame mara moja (kwa haraka) kwani anaweza kujeruhiwa zaidi.
Hivyo ukikutana na mzee aliyeanguka na ukishuku kwamba amevunjika mifupa yake, bora usimwinue mwache na usubiri gari la wagonjwa, lakini akitokwa na damu, bora umsaidie kuzuia kutoka na damu kwanza
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv


 
Top