Wanawake walio wengi wanalalamika kila kukicha wakidai wapenzi wao wanawakimbia hila mimi naweza kusema kabla haujasema umekimbiwa kwanza angalia wewe umemfanyia nini mpaka ulalamike na Unaambiwa raha ya penzi ujue kuenzi, Je mpenzi wako unamfurahisha kwa mambo yapi? basi leo nikuibie siri Jinsi ya Kumfurahisha Mwanaume wako katika mahusiano yenu.
KUWA KARIBU NAE,
Unapoanzisha uhusiano ujue kabisa kile ni kitendo kisichokuwa cha hiari jitahidi mara moja moja unamridhisha mwenzi wako sio kila siku uko bize na shughuli za hapa na pale wenzio wakichangamkia fursa ujue itakula kwako na usiposhtuka mapema utajikuta unasubiri Meli Airport.
ISHI NAE KWA AMANI,
Kuna watu wanajikuta wanataka kubembelezwa tu pasi na sababu atatafuta sababu ilimradi tu atake kujua kwamba akimuudhi mpenzi atachukua uamuzi gani, angalia kuna wengine hawajui kubembeleza kwa kingereza tunawaita “unromantic men” yaani huyu ukimzingua tu inakula kwako.
USICHUNGUZE SIMU YAKE,
Mahusiano ya kipindi hiki cha utandawazi yamegeuzwa thamani yake kuwa ni sawa na utamu wa bazoka unatafuna ikiisha utamu unatema lakini chanzo cha yote ni simu za mkononi kwani zimechochea sana usaliti hasa huu mtandao ulioteka vijana wa sasa “Whatsapp” mtu akitumiwa picha tu hata mtu hujawahi kumuona ushaingiwa tamaa. Ili kuepukana na presha zote hizo achana na kukagua simu ya mwenzi wako yaani kwa lugha nyepesi acha shobo na simu ya mwenzio maana isije kuwa chanzo cha kuhatarisha uhusiano wako na wanaume wengi hawapendi kwa kuzingatia hilo atakupenda mno.
MLISHE AU JENGA MAZOEA YA KULA PAMOJA NAE,
Hivi wewe hapo ukilishwa huwa unajisikiaje? Bila shaka jibu ni raha tupu asikwambie mtu mwanaume ni kama mtoto jitahidi kuenda nae sawia kwa mahaba haya akikuacha basi huyo ujue kivuruge. Kuna wengine hudai kuwa wanaostahili kulisha ni wale wanaotembea na waliowazidi umri la hasha! Utafeli dada wewe utaishia kuambiwa niko bize na kazi tutaonana wikiendi.
USIMSUMBUE NA MIZUNGUKO YAKE,
Kuna wanawake wengine huwa wanaboa sio siri kwa hili badilikeni mtu atataka ajue unaenda wapi na unafanya nini na uko na nani tena wengine hufika mbali “ooohooo uko na nani mbona huongei kwa kujiachia hebu ni kiss nijue kama hauko na mwanamke” tambua yule ni mtu mzima anamajukumu yake sio kila kitu akwambie vingine kubali vikupite asikudanganye mtu mwanaume hapendi kufatiliwa kupita kiasi.
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv


 
Top