Watu wengi wamekua wakitamani jinsia flani za watoto ili wazae watoto wachache ila kukosa kwa jinsia waliyoipanga hujikuta wakizaa watoto wengi wakati wakitafuta jinsia husika, mpaka familia hugombana na kutengana .unaweza kujiuliza Nini nifanye ili nipate mtoto wa kike au kiume? Je kuna dawa au vyakula vya kusaidia kupata mtoto ninayemtaka?Siku gani nikikutana na mwenzangu naweza pata mtoto wa kiume au kike?
Na maswali mengine mengi huonesha shauku kubwa ya kupata mtoto wa jinsia uipendayo. Tuanzie hapa.
Tuanze na  Jinsia ya Mtoto
Mtoto hutengenezwa pale mbegu ya kiume inapokutana na yai la kike. Mbegu za kiume hubeba vinasaba vya X na Y, wakati yai la mwanamke likiwa na vinasaba vya X peke. Ikikutana mbegu ya kiume yenye kinasaba cha X na yai la kike (yenyewe yana vinasaba vya X peke yake) mtoto wa kike hutungwa. Mbegu ya kiume yenye kinasaba cha Y Ikikutana na yai la kike, mtoto wa kiume hutungwa.
(Mbegu ya kiume Y + Yai la kike X = Mtoto wa Kiume)
(Mbegu ya kiume X + Yai la kike X = Mtoto wa Kike)
 
Na hizi ni Njia za Kupata Mtoto Wa Jinsia Uipendayo
Mbegu za kiume zenye vinasaba vya Y huwa ni nyepesi, husafiri kwa haraka katika via vya uzazi vya mwanamke na huishi kwa muda mfupi ukilinganisha na mbegu zenye vinasaba X. Zenye vinasaba X huwa nzito zaidi, huenda polepole na huishi kwa muda mrefu zaidi.
Hivyo, kinadharia ili kupata mtoto wa kiume unaweza ukakutana na mwenza wako siku ambayo yai la uzazi linatoka (ovulation), kwani mbegu Y zitasafiri haraka na kukutana na yai ili kulirutubisha kuwa mtoto wa kiume.
Mtoto wa kike, kutana na mwenzi wako siku 2 au 3 kabla ya yai kutoka. Kwa sababu mbegu Y huishi kwa muda mfupi, nyingi zitakufa wakati zinasubiri yai huku mbegu X zikiwa kwa wingi mpaka siku yai linatoka. Yai likitoka mbegu X zitakuwa kwa wingi kuungana na yai kutunga mtoto wa kike.
Kiuhalisia, sio rahisi kufanikisha hilo.

Na kwa wakati mwingine waweza kufanya hivi
Kuna njia mbalimbali zinazosemekana zinaongeza uwezekano wa kupata mtoto wa kiume au kike. Njia hizi inajumuisha kula vyakula vya aina fulani, mikao maalumu ya kimapenzi, kuweka vitu sehemu za siri na nyingine nyingi bado haziwezi kutatua tatizo hili.
Mpaka sasa na maendeleo yote ya kiteknolojia hatujaweza kupata njia ya kuwezesha kupata jinsia ya mtoto unayoitaka. Ni majaliwa ya Mwenyezi Mungu!

 JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top