Kuna vitu unaweza kuamini na vingine unaweza kuamini lakini kutokana na tafiti hizi tunaweza kuamini katika ulimwengu huu. Amini usiamini panya ni kiumbe wa ajabu ambaye wengi humhofia kutokana na tabia yake ya kung’ata na kupuliza; ni kiumbe pekee anayeweza kukung’ata na maumivu yake ukaja kuyasikia baadae kabisa. Lakini si hilo tu pia kiumbe huyu huogopwa kwa uchafu na hasa ugonjwa wa tauni.

Lakini tofauti na unavyofikiri panya ni mnyama wa kupendeza kwani utafiti mpya umebaini wanapenda sana kucheka. Watatifi kutoka Chuo Kikuu cha Humboldt cha Ujerumani wamegundua ubongo wa panya una neva inayohusiana na vitendo vya kucheka.

Watafiti Shimpei Ishiyama na Michael Brecht wamepima shughuli za neva husika kwenye ubongo wa panya na kutafiti mabadiliko ya shughuli hizo kabla na baada ya kuwashwa. Utafiti unaonesha panya wakiwashwa, wanacheka sana na kucheza dansi kama waliofurahishwa, na inaonekana kwamba hata panya wanajua mikono ya binadamu itawawasha. Lakini vicheko vyao ni vya ‘ultrasonic’ na havisikiki na binadamu. Kabla ya hapo wanasayansi walifikiri neva hizi zinahusiana na hisia ya kugusa tu, lakini utafiti huo mpya unaonesha kuwa neva hizi pia zinahusiana na hisia ya furaha.

Pia watafiti wamejaribu kuchochea neva husika za panya badala ya kuwafanya wawashwe moja kwa moja, majaribio yanaonesha kuwa neva hizi zikichochewa pia panya wanacheka.

Lakini panya wakiwa katika hali ya wasiwasi kwa mfano wakiwekwa kwenye mahali pa juu sana, kuwawasha au kuchochea neva zao hakutawachekesha. Wanasayansi wamesema jambo hili huenda linamaanisha kuwa mmoja akicheka baada ya kuwashwa hakika ana furaha moyoni.

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv


 
Top