Labda kwa wale wasiofahamu niwaambie tu kwamba, dhana ya mapenzi ina wigo mpana na ndiyo maana hutasikia hata siku moja ‘TUMEPUMZIKA’ kuyazungumzia. Hata hivyo, tunachofanya siku zote ni kukumbushana kwa yale tunayoyafahamu na kushauriana pale tunapohisi wengi hufanya makosa.
Hakuna kitu kinachoumiza katika uhusiano wa kimapenzi kama kusikia mpenzi wako anatembea na mtu mwingine tena ambaye huenda unamfahamu, inauma kupita maelezo; mbao wamewahi kusalitiwa wanajua machungu yake.
Kwa kifupi kasi ya kusalitiana kwa wapenzi imekuwa ikiongezeka kila uchwao kiasi kwamba unapoingia katika uhusiano wa kimapenzi unahisi kama unaingia kwenye matatizo makubwa. Hii ni kwa sababu watu sio waaminifu kwa wapenzi wao.
Unaweza kuwa na mpenzi wako ambaye kila mnapoonana anakueleza kuwa, anakupenda, anakujali, hawezi kukusaliti na atakuwa na wewe katika shida na raha. Lakini huyo huyo usishangae siku moja ukamkuta yupo na mtu mwingine. Swali la kujiuliza ni kwamba, kwa nini wapenzi wanasalitiana?
Zipo sababu nyingi sana zinazowasukuma baadhi ya watu kudiriki kuwaumiza wenza wao kwa kuchepuka nje ya mahusiano . Hata hivyo, leo nataka kuzungumzia namna tamaa ya fedha na ya kimwili vinavyochangia katika hili.
Kwa wale ambao wapo kweye ndoa wakati mwingine, hasa wanawake wasipopatiwa mahitaji muhimu na akatokea jamaa na kumhakikishia kumpatia kila anachotaka, wanakubali mara moja bila kujua kwamba wao ni wake za watu ama wapenzi wa watu na kujikuta wanajenga mazoea.

Wengine wanapatiwa kila kitu na waume zao lakini sasa kinachotokea ni tamaa za kimwili tu ambazo zinawasumbua na kujikuta wanatafuta waume wengine huku wakidai kuwa, wanatafuta ladha tofauti. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top