Miongoni mwa vitu vinavyofanya watu waishi maisha mazuri sana duniani ni vipaji walivyo jaaliwa na mwenyezi mungu na inakuwa furaha sana pale unapoishi ndani ya ndoto yako kutokana na kipaji ulichopewa kwanza jiulize yafuatayo wazazi au walimu wako wameshawahi kugundua uwezo wako katika kipaji cha jumla mfano taaluma, michezo, kuzungumza, nk? Ulishawahi kujulishwa au kupata tetesi? mpaka sasa kipaji hicho kimeshajitokeza na kukufanya uwe na mahala pamoja unapofanya vizuri zaidi ? kama ndiyo tumia fursa hiyo kipaji kitatokeza.
Chunguza mazingira yako, 
angalia mazingira ya unachofanya kama yalitokana na uwezo wako wa asili au ulijiingiza kwa kuhamasishwa na mtu, shida, au tamaa ya kutajirika haraka. Tafuta kile kinachotokana na uwezo wako wa asili ili kipaji chako kiweze kufanya kazi.
Angalia ulichokuwa unakifanya, 
angalia kama kuna ulichokuwa ukikifanya hapo zamani ambacho hata kama hukukifanya kwa ufanisi kwa kukosa maarifa lakini kilikupa upekee lakini kiwe kilitokana na uwezo wako wa asili na ulifanya mara kwa mara. Kiendeleze na baada ya muda kitakupa mwelekeo wa wapi uende na hivyo kufanya uwe tofauti na wengine.
Nini kilikutambulisha na kinachokutambulisha, 
angalia katika unavyovifanya au ulivyovifanya ni kipi kilikutambulisha au kinakutambulisha na kukufanya ukubalike kipekee na sio kutokana na kiwango chako cha kisomo. Kipaji halisi hakitegemei kiwango cha kisomo, bali uwezo wa asili ndio hutawala katika kutenda jambo. Katika kiwango chochote cha elimu bado uwezo wa asili utachukua nafasi na kutawala katika utendaji na kukufanya wewe ndiyo upate sifa na sio elimu yako.
Ni nani aliyekwambia una Kipaji?, 
jiulize kama umeshawahi kuambiwa una kipaji? Je ni kipaji gani? Umeshawahi kuambiwa mahala kwingine na hapo maneno kama hayo? Hicho ndicho unachokifanya mara kwa mara kwa ufanisi kuliko mengine?.
Tazama hisia zako, 
angalia kama unachofanya unahisia nacho au unafanya kwa sababu hauna kazi nyingine? Na hisia zako za ndani zinasemaje? Jali zaidi hisia zako za ndani sana zinazohusiana na uwezo wako bila kujali vitisho kwa sababu kipaji kina nguvu kuliko kitisho chochote kilichoko mbele yako.

Kama wewe hujawahi kuhisi au kusikia chochote kuhusu kipaji chako basi ni kwa sababu ya kukosa nafasi ya kukionyesha. Fanya kila unachohisi kinatokana na uwezo wako wa asili hata kama kimewahi kufanywa na mtu mwingine 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top