Kwa walio wengi sasa hasa madada wanapenda sana kupiga selfi yaani picha za kujipiga mwenyewe kwa baadhi ya madada selfie ndio kila kitu utafikiri walisoma photojournalism; yani kila mara popote alipo ni kujitwanga picha na hivi siku hizi kuna powerbank ndio kabisaa hawahofii kwamba simu itazima.
Sasa taarifa ikufikie wewe mpenda picha za selfie kwamba takwimu za utafiti uliofanyika hivi karibuni juu ya vifo vinavyochangiwa na upigaji picha vimekuwa vikiongezeka kila uchwao kwani mwaka 2014 walikufa watu 15, 2015 wakafariki watu 39 na mwaka huu kwa kipindi cha miezi nane ya awali tayari wamefariki watu 73.
Utafiti uliofanywa na Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu Hemank Lambawa akishirikiana na wenzie wa Chuo Kikuu cha Carnegie Mellon huko Pittsburgh umegundua njia ya kukabiliana na vifo hivyo ni kutengeneza App maalumu itakayokuwa ikitoa ishara mara mtumiaji awapo kwenye hatari ili aweze kujihami.

Tazama baadhi ya picha ambazo watu wamekuwa wakipiga selfie licha ya kuwa kwenye hatari ya kupoteza maisha.

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top