Tukiangalia Katika ulimwengu wa mapenzi kuna mambo kadha wa kadha yanayo weza kusababisha watu wazima kuamua kuingia kwenye mahusiano na watu wenye umri mdogo.
Leo edonetz tunaangazia sababu za watu wenye umri mkubwa kupenda kuwa kwenye mahusiano na watu wenye umri mdogo na kinyume chake.
URAHISI WA MAISHA – 
Vijana wengi wakileo wanapenda mteremko; mara nyingi hupenda maisha ya bwerere yaani mteremko pasipo kujishughulisha. Mara nyingi hupenda vya bure na kuamua kuingia kwenye mahusiano na mtu aliyemzidi umri kupita kiasi na hii inatokana na baadhi yao kuwa katika hali ya ugumu wa maisha.
PESA
imekuwa na ushawishi mkubwa katika suala zima la mahusiano. Mabinti wenye umri mdogo wamejiingiza katika mahusiano wa wanaume wenye umri mkubwa sambamba na vijana wakiume wenye umri mdogo kupenda kulelewa na wamama waliowazidi umri ili kujipatia pesa.
KUEPUKA USUMBUFU. 
Hapa mabinti wengi huamini njia pekee ya kuepuka msongo wa mawazo katika mahusiano ni ‘kudate’ na wanaume wenye umri mkubwa kuliko wao kwa kuwa wanaamini hawapepesi macho kama vijana wenye umri sawa na wao. Pia wanaamini wanaume wenye umri mkubwa hawana wivu wala muda wa kuwa fuatilia nyendo zao kila mara.
UHITAJI WA MTOTO 
kwa kuwa na hakika ya kuwalea kutokana na uwezo wa kipesa walionao. Vijana wa kiume wa nyakati hizi huepuka kuzaa na mabinti kwa kuwa hawapendi majukumu, hupenda starehe ndio maana hupendelea kulelewa.
KUFUATA RAHA YA PENZI 
ambayo inadaiwa kuwa wanaikosa kutoka kwa waume zao halikadhalika Inasemekana wamama hupenda vijana ambao damu inachemka ili kufurahia raha ya penzi. 
MALUMBANO NDANI YA NDOA  YALIYO SUGU.
Magomvi na kero zinazoibuka siku hadi siku husababisha mwanamke/mwanaume  kutafuta binti ama kijana mbichi atakaye mtuliza moyo na kumsahaulisha machungu anayo yapata ndani ya ndoa.
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv


 
Top