Mapaja  ya ndani na makwapa hutokea weusi kutokana na msuguano wa ngozi kwasababu ya mapaja kugusana, hata ngozi iliyokauka pia inaleta weusi katika ngozi.
Hivyo nimekuletea njiaasili ya kuondoa weusi huo bila kutumia madawa makali.

TUMIA MAFUTA YA NAZI NA NDIMU.
Mafuta ya nazi yanatumika kulainisha ngozi lakini unaweza kutumia pia katika kuondoa weusi ukichanyanya na ndimu..fuata hatua hizi::
*Chukua vijiko 3 vya mafuta ya nazi changanya na ndimu nusu
*Paka sehemu yenye weusi katika mapaja huku ukisugua kama unafanya massage kwa dakika 15.
*Kisha osha na maji ya uvuguvugu na kausha kwa kitambaa kilaini na kisafi.

TUMIA MCHANGANYIKO WA SUKARI ASALI NA NDIMU.
 
Mchanganyiko huu pia unaweza ukaondoa weusi katika mapaja na makwapa, fuata hatua hizi::
*Changanya kijiko kimoja cha asali, ndimu nusu na kijiko kimoja cha sukari.
*Paka sehemu yenye weusi na sugua kawaida hadi sukari ipotee.
*Acha ikae kama dakika 10 kisha osha na maji ya uvuguvugu.

GANDA LA CHUNGWA NA ASALI
Kama mnavyojua machungwa yana vitamin C, na hivyo ukichukua ganda la chungwa pamoja na asali, mchanganyiko wake pia unaondoa weusi. Fuata hatua hizi::
*Chukua ganda la chungwa na kijiko kimoja cha asali.
*Kamua hilo ganda maji yake yangie kwenye asali.
*Kausha nakusaga hilo ganda kisha poda yake ichanganye na asali
*Paka mchanganyiko huo katika sehemu yenye weusi, kaa kwa muda wa dakika 15

*Osha na maji ya kawaida hadi kugandaganda kupotee. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top