Wataalamu wa afya husema ubongo wa binadamu hufanya kazi kwa msukumo wa hali ya hewa na mazingira kwa ujumla, kwa mfano kukiwa na  hali ya mvua ubongo utatafakari jambo kulingana na hali ya hewa ilivyo kupitia milango ya fahamu na kama ni jua kali vivyo hivyo ubongo utafanya maamuzi kulingana na hali ya hewa ilivyo.
Inashauriwa mara tu unapoamka jambo la kwanza unapaswa kujinyoosha viungo ili kuuweka mwili sawa kwani mawazo chanya hupatikana katika hali ya hewa iliyotulia mathalani kwenye miti mingi ambapo hewa safi hupatikana, kwenye milima na maporomoko ya maji au maeneo yenye uoto wa asili.
Wanasaikolojia wanautaja uoto wa asili kama njia bora ya kutibu mtu anayesumbuliwa na msongo wa mawazo kwa kuikutanisha akili na uoto wa asili; mbali na njia ya kumfanyia ‘cancelling’, mtu huyu anapopata fursa ya kukaa maeneo yaliyotulia na yenye hewa safi kwa kiasi kikubwa husaidia kupunguza ama kuondoa kabisa msongo wa mawazo.

Mara nyingi hushauriwa kutembelea maeneo ya mbuga za wanyama, kwenye milima, chemchem, mito, bahari, maziwa na maeneo yaliyozungukwa na miti mingi.Msongamano uliopo maeneo ya mijini unaosababishwa na uhaba wa ajira, huchangia msongo wa mawazo kutokana na hali ya joto ambalo ni zao la moshi na mvuke kutoka viwandani pia kelele za magari, wapiti njia pamoja na magari. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top