Wengi wetu, tunatumia mikono kuosha uso…si ndiyo? Lakini unachotakiwa kujua ni kuwa mikono yetu hata kama huwa una nawa kwanza bado inakuwa na bacteria kwenye kucha na vidole.

Kwenye urembo si salama sana kutumia mikono yako. Kwahiyo ni vizuri ukatumia kitambaa maalumu kwaajili ya kujisafshia.Tafuta kitambaa kilaini na kisafi ndio uwe unatumia kuoshea uso wako.

Osha uso wako mara 2 kwa siku, kama unavyopiga mswaki mara 2 kwa siku. Asubuhi na usiku kabla hujalala, hakikisha unatoa makeup yote vizuri. Hata kama haupaki makeup osha uso wako kuondoa jasho, mafuta na vumbi.
Wakati wakuosha uso wako usisahau hii sehemu ya juu yani eneo la komo.Usisahau  
Wengi huwa hawaoshi vizuri uso sehemu ya paji la uso wakiogopa kulowanisha nywele zao au kuharibu style waliyoiweka.
Unachotakiwa kufanya ni kutafuta kofia ambayo utakuwa unavaa ili kuondoa nywele usoni na hakikisha unaosha uso wako vizuri.

Ukipata vitambaa vyakuoshea uso vile vinavyotumika kwaajili ya watoto ni vizuri zaidi kwani vinakuwa na pamba. pia unaweza kutumia kusafishia uso wako, ila hakikisha ni 100% cotton.

Kuna wale pia wanaotumia mabrush au yapo ya aina nyingi kwahiyo unashauriwa kubadilisha brush zake angalau kila baada ya mwezi au miez 2 na uchague brush laini. Chagua sabuni itakayokufaa wewe kutokana na aina ya ngozi yako. 
Tumia maji ya uvuguvugu na usisugue. Baada ya kuosha tumia taulo safi kukausha uso wako. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top