Napenda kusisitiza kuwa miguu ni sehemu ambayo inatakiwa kutunzwa kwa upekee kama ilivyo sehemu nyingine ya mwili kama uso, haijlishi miguu yako ni miembamba au minene iwapo utaitunza vizuri sina shaka kuwa utavutia kwa nguo yoyote utakayoivaa.
Kuna njia nyingi za kutunza miguu na unaweza kutunza miguu yako hata kama huna fedha za kununulia vikorokoro vinavyotakiwa. fanya hivi:
Chukua beseni na kuweka maji ya uvuguvugu yenye povu la sabuni maalum ya kuoshea miguu kisha loweka miguu na iache kwenye maji kwa muda wa robo saa hivi.
Chukua aina ya scrub uliyoichagua kwa ajili ya miguu yako paka na ikikauka anza kusugua miguu yako hadi kwenye vidole na unyayo, kisha jisafishe kwa maji ya uvuguvugu.
Pia unaweza kutumia baadhi ya vitu unavyoweza kutumia ili kuitengeneza miguu yako na vinapatikana kwenye maduka yote ya vipodozi na hapo usikurupuke ulizia kwa wataalamu ili upate maelezo ya jinsi ya kuvitumia.
Pia unaweza kutembelea baadhi ya saluni ambazo zinatoa huduma hiyo jitahidi hata mara moja kwa mwezi kuhakikisha miguu yako inapata huduma nzuri ili iwe ya kuvutia.
Kwa wale ambao miguu yao ni makovu au madoadoa wajaribu kutumia scrub na kama hawatafanikiwa kuondoa tatizo hilo basi wanashauriwa kutumia cream na sabuni zenye mchanganyiko wa ukwaju kwani zinasaidia sana kuondoa madoa.

Pia unaweza kuchukua ukwaju ukaloweka kwenye maji ukishalainika changanya mchanganyiko huo na asali kisha paka kwani husaidia kuondoa madoa kwenye miguu. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top