Tangu utotoni, watoto wasichana hufunzwa jinsi ya kujiweka safi na nadhifu wakati wote.Usafi huu pia unahusu sehemu nyeti; hakuna mwanamume atakubali kuwa karibu na mwanamke anayetoa uvundo Uke wa mwanamke ni moja ya maeneo muhimu sana yanayohitaji kutunzwa kwa kiwango cha hali ya juu
Ni nyakati gani muhimu ambazo mwanamke anastahili kuwa mwangalifu zaidi na kuosha sehemu nyeti;
1. Kabla na baada ya kushiriki mapenzi
Unashauriwa kuosha kisima chako kabla na baada ya kushiriki mapenzi ili kiwe kisafi. Wataalamu wanasema mume na mke wote kwa pamoja wanastahili kuoga kabla na baada ya kushiriki ngono ili kuzuia  maambukizi ya bacteria, kuvu na virusi.
 Oga kabla na baada ya kula ngoma.
Kabla kuanza kushiriki mapenzi hakikisha umeweka karibu taulo kadha safi. Mwanamke hufaa kujipangusa mara tu jamaa akiondoa mtutu wake ili kuondoa mabaki ya manii, chembechembe za manii na umajimaji mwingine ambao hupatikana wakati huu. Kisima hupata mikwaruzo midogo midogo wakati wa ngono na hivyo kutumia sabuni na vitu vingine vilivyo na kemikali hudhuru sehemu hii nyeti.
2. Wakati wa hedhi
Ni haraka sana mwanamke kutoa uvundo wakati wa hedhi iwapo hatadumisha usafi wa kisima chake. Huhitaji kufanya mambo mengi kando na kuoga mara kwa mara, kuoga mara mbili kwa siku kunatosha kukuweka msafi.
Jinsi ya kudumisha usafi zaidi wakati wa hedhi.
Osha tupu yako kwa maji safi peke yake; usitumie sabuni pengine tu kwenye kinena kuondoa uchafu wa damu. Vaa sodo yako lakini hakikisha unaibadilisha mara kwa mara; haifai kulowa kupita kiasi kwani uvundo wa damu utaanza kujitokeza na vile vile kuna hatari ya kujiletea maambukizi. Iwapo huna tatizo lolote kushiriki ngono wakati huu, hakikisha unatandika taulo kadha kitandani usichafue shuka na unajiosha mara tu baada ya shughuli.
3. Baada ya kukojoa
Hapa si lazima kutumia maji lakini yakiwepo ni bora zaidi. Hakikisha kipochi chako kiko na tishu wakati wote. Kila unapoenda msalani, iwe kwa haja ndogo ama kubwa, pangusa tupu yako.
Hakikisha unajipangusa kila unapoenda haja ndogo na kubwa. Pangusa kutoka mbele ukienda nyuma ili usieneze bakteria kwenye tupu na hivyo kujiletea maambukizi. Kitendo hiki kitasaidia kukuweka mkavu na msafi siku nzima.
4. Kila siku kama ilivyo desturi

Kuoga ni kila siku, vilevile kusafisha sehemu yako nyeti ni jambo la kila siku. Osha tupu kwa maji safi; safisha kinene vizuri kabisa baada ya kukiosha kwa sabuni. Siku zingine unashauriwa kutovaa chupi, keti chini na upanue miguu ili hewa safi iingie humo!

JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top