Tangu utotoni, watoto wasichana hufunzwa jinsi ya kujiweka safi na
nadhifu wakati wote.Usafi huu pia unahusu sehemu nyeti; hakuna mwanamume
atakubali kuwa karibu na mwanamke anayetoa uvundo Uke wa mwanamke ni moja ya maeneo muhimu sana yanayohitaji
kutunzwa kwa kiwango cha hali ya juu
Ni nyakati gani muhimu ambazo mwanamke anastahili kuwa mwangalifu
zaidi na kuosha sehemu nyeti;
1. Kabla na baada ya kushiriki mapenzi
Unashauriwa kuosha kisima
chako kabla na baada ya kushiriki mapenzi ili kiwe kisafi. Wataalamu wanasema
mume na mke wote kwa pamoja wanastahili kuoga kabla na baada ya kushiriki ngono
ili kuzuia maambukizi ya bacteria, kuvu
na virusi.
Oga kabla na baada ya kula
ngoma.
Kabla kuanza kushiriki
mapenzi hakikisha umeweka karibu taulo kadha safi. Mwanamke hufaa kujipangusa
mara tu jamaa akiondoa mtutu wake ili kuondoa mabaki ya manii, chembechembe za
manii na umajimaji mwingine ambao hupatikana wakati huu. Kisima hupata
mikwaruzo midogo midogo wakati wa ngono na hivyo kutumia sabuni na vitu vingine
vilivyo na kemikali hudhuru sehemu hii nyeti.
2. Wakati wa hedhi
Ni haraka sana
mwanamke kutoa uvundo wakati wa hedhi iwapo hatadumisha usafi wa kisima chake.
Huhitaji kufanya mambo mengi kando na kuoga mara kwa mara, kuoga mara mbili kwa
siku kunatosha kukuweka msafi.
Jinsi ya kudumisha usafi zaidi wakati wa hedhi.
Osha
tupu yako kwa maji safi peke yake; usitumie sabuni pengine tu kwenye kinena
kuondoa uchafu wa damu. Vaa sodo yako lakini hakikisha unaibadilisha mara kwa
mara; haifai kulowa kupita kiasi kwani uvundo wa damu utaanza kujitokeza na
vile vile kuna hatari ya kujiletea maambukizi. Iwapo huna tatizo lolote kushiriki ngono
wakati huu, hakikisha unatandika taulo kadha kitandani usichafue shuka na
unajiosha mara tu baada ya shughuli.
3. Baada ya kukojoa
Hapa si lazima kutumia
maji lakini yakiwepo ni bora zaidi. Hakikisha kipochi chako kiko na tishu
wakati wote. Kila unapoenda msalani, iwe kwa haja ndogo ama kubwa, pangusa tupu
yako.
Hakikisha unajipangusa kila unapoenda haja ndogo
na kubwa. Pangusa kutoka mbele
ukienda nyuma ili usieneze bakteria kwenye tupu na hivyo kujiletea maambukizi.
Kitendo hiki kitasaidia kukuweka mkavu na msafi siku nzima.
4. Kila siku kama ilivyo desturi
Kuoga ni kila siku,
vilevile kusafisha sehemu yako nyeti ni jambo la kila siku. Osha tupu kwa maji
safi; safisha kinene vizuri kabisa baada ya kukiosha kwa sabuni. Siku zingine
unashauriwa kutovaa chupi, keti chini na upanue miguu ili hewa safi iingie
humo!
JIUNGE
NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz , twiter@edonetz , inst@edonetz_blog na youtube@edone tv