Uzito mkubwa wa kupindukia ni tatizo
kubwa la kiafya katika maisha yetu ya kisasa. Uzito unapozidi kiwango ambacho
kinahitajika kwa mtu husika kunachangia matatizo mengi ya kiafya.
Baadhi ya matatizo yanayosababishwa
na uzito mkubwa ni Kisukari ,Shinikizo la Juu la Damu na magonjwa mengine ya
moyo.
Sababu za Kuongezeka Uzito wa Mwili:
Uzito mkubwa wa kupita kiasi
unatokana na kuongezeka kwa mafuta mwilini ambayo hutunzwa sehemu mbalimbali
mwilini kama juu ya ngozi,tumboni na juu ya viungo vya nadni vya miwili kama
moyo,utumbo nk. Pia hujenga utando pembeni mwa mishipa ya damu.
Mafuta hutunzwa kama akiba pale mtu
anapokula chakula kingi kuliko kiasi cha nguvu anazohitaji na hivyo mwili
unabadilisha chakula hicho kuwa mafuta na kuweka katika akiba.
Watu wa mijini wananenepa zaidi
kuliko wa vijijini kwasababu ya mitindo yetu ya maisha ambayo tunakula chakula
kingi na chenye mafuta lakini hatuifanyishi miili yetu kazi za kutosha kutumia
nguvu tulizoingiza.
Chukua mfano,
mtu anakula kJ 5, mchana anakula kJ 20, jioni kJ 15 jumla ni Kj 40. Anaenda
kazini kwa gari,anakaa masaa 8 kwenye kiti kazini kisha jioni anarudi na gari
hadi nyumbani kwake. Umabali aliotembea ni mita 10-20 jumla ya nguvu ulizotumia
jouli 30, nguvu zilizobaki bila matumizi ni kJ 10.
Sasa mwili unafanya nini na kJ 10
zilizobaki? Zinahifadhi kwa matumizi ya baadae kama mafuta ambayo hatakuja
kuhitaji. Fikiria inakuwaje katika siku 30 za mwezi na hifadhi hii. Hivi ndivyo
uzito na unene unavyopatikana. * kJ=Kilo Jouli
(Kipimo cha nguvu mwilini)
unaweza Kupunguza Uzito wa Mwili namna hii.
1.
Kupunguza
kiasi cha chakula kwa siku
Hii ni njia moja kubwa ya kufanya
usipate uzito mkubwa na pia kupunguza uzito. Kama unahitaji kJ 30 kwa siku basi
kama una uzito uliozidi utatakiwa kula kJ chache mfano kJ25 ili kJ 5
zinazohitajika zitoke katika akiba ya mafuta mwilini. Uzito mkubwa unachangiwa
kwa asilimia nyingi na kiasi kikubwa cha chakula mtu anachokula. Naomba ifahamike
kuwa suluhisho sio kuruka mlo,unatakiwa kula kila mlo ila kwa kiasi kidogo.
2.
Kufanya
Mazoezi ya Mwili
Mazoezi ya mwili iwe kwa kufanya
kazi au kwa kukimbia au katika vituo vya mazoezi au nyumbani yanasaidia
kupunguza uzito kwa kuunguza mafuta ya akiba katika mwili. Mfano kama unakula
kiasi unachohitaji tu kwa kazi za kawaida na kisha ukafanya mazoezi,mwili
utahitaji kuchukua nguvu toka katika mafuta ili kujazia upungufu. Mfano unaweza
ukatumia kj 10 kwa mazoezi ya dk 30 mpaka dk 60. Hivyo ukifanya mara kwa mara
kama si kila siku utapungua tu uzito.
Mazoezi rahisi kufanya ni kukimbia
kila jioni au asubuhi kwa umbali wa km 1 mpaka 2 zinatosha. Lakini unaweza
kwenda katika kituo cha mazoezi jioni au ukanunua vifaa vya mazoezi na kufanya
nyumbani kama unaweza.
3.
Mpango
Sahihi wa Chakula-Chagua Kula Chakula Sahihi
Katika njia ya kwanza nimesema juu
ya kiasi unachokula,hapa naelezea juu ya aina ya chakula unachotumia
kinachangia uzito kuongezeka au vinginevyo. Ulaji wa vyakula vingi vya wanga na
mafuta ni chanzo kikubwa cha unene na uzito kuongezeka. Vyakula kama
ugali,wali,mkate mweupe,bia na pombe za kienyeji zinazotokana na wanga (kimea)
huchangia kuongezeka kwa uzito. Matumizi ya aina hii ya chakula ni muhimu
kupunguzwa katika mlo wako.
Fanya hivi katika mpango wa
chakula:
- Acha kula Vyakula vya Sukari
Sukari inayozidi mwilini toka katika
vyakula hubadilishwa na kuwa mafuta. Vyakula kama chokuleti,biskuti,keki na
vinyaji kama soda vina kiwango kikubwa cha sukari. Pia usitumie sukari nyingi
katika chai na juisi.
- Kula Mboga Mboga na Matunda Kwa Wingi
Mboga mboga ni nzuri kwa afya kwa
ujumla lakini pia haina mafuta hivyo itakufanya kuingiza mafuta kidogo mwilini.
Matunda halikadharika hayapunguzi uzito moja kwa moja bali yatakufanya ushibe
na usitamani kula kila mara kwani yanakata hamu ya chakula. Hivyo utaokoka na
tabia ya kula kila mara ambayo huchangia sana kuongezeka uzito.
- Acha Kula Kula Ovyo Nje ya Milo Maalumu
Uzito na kula kula hovyo ni marafiki
wakubwa. Ukiona mtu ni mnene ujue anapenda kula. Ile kweli anakulakula
ikimaanisha anakula kila mara na kila wakati chakula kinapokuwepo.
Anza leo kujenga tabia ya kula
kidogo na katika milo muhimu mitatu.
- Punguza Matumizi ya Chumvi
Ndiyo,chumvi inaongeza uzito.
Sodiamu iliyomo katika chumvi inachangia katika mchakato wa kikemikali
unaopelekea kuongezeka uzito. Tumia chumvi katika kiwango kidogo.
- Tumia Chai ya Kijani
Umesikia
kuhusu chai ya kijani (Green Tea), ni chai ambayo ni ya kijani
na inasaidia kuondoa sumu za mwili (antioxadation). Hii inasaidia katika
kusaidia mwili kuunguza mafuta katika njia inayoitwa thermogenesis.
- Tumia Chai ya Tangawizi
Tangawizi kama ilivyo chai ya kijani
inafahamika kuongeza mmeng’enyo wa chakula tumboni hivyo kupunguza mrundikano
wa mafuta yasiyotumika
- Kunywa Maji Mengi
Maji yanachangia kuharakisha mfumo
wa uvunjaji chakula tumboni na hivyo kupunguza mafuta yanayohifadhiwa.
JIUNGE
NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz , twiter@edonetz , inst@edonetz_blog na youtube@edone tv