Ni wazi kwamba katika migogoro mingi ya mahusiano simu imekuwa kichocheo kikubwa cha wapendanao au wanandoa kugombana. Simu ndizo zinazoleta uhasama na kuvunja ndoa nyingi. Simu ndizo zinawafanya watu wengi waliopo kwenye uhusiano kugombana.
Miaka ya nyuma, hususan wakati simu za mkononi zilipokuwa hazijaingia nchini, matatizo kwa wanandoa au wapendanao yalikuwa machache sana kulinganisha na sasa baada ya ujio wa simu.
Bahati mbaya sana, kati ya kesi nyingi za simu, zipo ambazo zinakuwa na ukweli lakini nyingine huwa hazina ukweli. Mtu anaanzisha ugomvi kwa sababu tu ujumbe wa kimahaba umeingia kwenye simu ya mke au mumewe. Hahitaji kuhoji. Atamtukana, atampiga na atafanya kila linalowezekana kuhakikisha anaondoa hasira zake kwa kile alichokiona.
Kumbe pengine angejipa nafasi ya kutafakari, akahoji, labda hata wasingefikia hatua ya kugombana. Anaanzisha ugomvi kumbe yule aliyetuma ujumbe huo, mwenzi wake wala hamjui.
KAMA WEWE NI MOJAWAPO  FANYA FANYA HIVI.
Suala la kwanza unalopaswa kufanya kabla hujaingia kwenye uhusiano, mchunguze vizuri mhusika. Hakikisha ni mtu mwenye moyo wa kuridhika.
Tunaposema moyo wa kuridhika maana Awe tayari ameshaamua kuwa ‘serious’ na mtu mmoja. Macho yake si ya kutangatanga. Hababaishwi na kila mwanamke au mwanaume amuonaye. Mtu wa aina hiyo hafai. Atakupotezea muda. Atakusababishia ugomvi kila wakati mbele ya safari. Anzisha uhusiano na mtu aliyetosheka na ujana.
UAMINIFU NI NGUZO KUU

Ukishafanikiwa kuwa na mtu mwenye sifa hizo, kinachofuata ni suala la uaminifu. Jenga imani kwa mwenzako. Mfikirie katika fikra chanya zaidi na si hasi. Muamini kwamba hawezi kukusaliti. Ukimuwazia mwenzako katika mazuri ni rahisi hata kukabiliana na wazushi watakaokuletea maneno ya uongo ili kukugombanisha na mwenzi wako. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top