Karibu msomaji wa edonetz katika makala ya kila siku na leo tuangazie katika suala la ndoa Matarajio ya wanandoa hasa wanawake katika ndoa zao huwa ni mali, starehe za kupindukia na mengine mengi kama alivyokuwa anayaona katika enzi za uchumba, lakini kwa bahati mbaya kuwa kwenye ndoa hakuna sehemu ya kuweka wazi maslahi binafsi basi husubiri kuona kama miujiza itatokea.
Lakini kwa walio wengi hujisahau jambo ambalo huifanya ndoa kuwa chungu na hatimaye kufarakana wakati ndoa ikiwa mbichi. Hila unahitajika umakini katika vitu vifuatavyo.
UPENDO
Upendo wa kweli ni jambo muhimu katika maisha ya ndoa, vijana wengi hukimbilia ndoa kisa mali hasa vijana wa kike, bila kusahau ndoa ni pingu za maisha na huyo mtu utakaa naye milele. Upendo wa kweli usipokuwepo katika ndoa haiita dumu kwani amani haitakuwepo, pia faraja kati ka wanandoa haitopatikana na ndoa hiyo hugeuka maigizo.
UVUMILIVU
Ndoa imeundwa na watu wawili ambao walitoka nyumba tofauti, malezi na maisha tofauti, ndoa huwajumlisha kutokana na tofauti zao, kabla ya ndoa kuna kitu kinachoitwa courtship (Uchumba) hiki ni kipindi ambacho wapenzi hujuliana tabia zao na kuunganisha tofauti zao na kawaida hutumia mwaka 1 mpaka 4 na ikizidi hapo ni tatizo, kukiruka au kukizidisha kipindi hiki huharibu ndoa nyingi na kama hapakuwa na maelewano ya tabia hapa mnaruhusiwa kuachana na kama ukilazimisa ndoa hiyo haitadumu.
UAMINIFU
Kama upendo wa kweli ukiwepo ndani ya nyumba, uaminifu hasa ndio huhitajika, kama hamta aminiana vitu vidogo vitawatenganisha, maana jamii kawaida huonea wivu ndoa na kutupa mishale ya maneno na matendo ili kuijeruhi ndoa, siri za ndani zinapaswa kuishia baina ya wanandoa, na kama uaminifu hauta kuwepo ndoa itakuwa mashakani  na nivigumu kudumu.
MSAMAHA
Kuna msemo wa Kiswahili unasema “hakuna aliye mkamilifu” hii inamaanisha kwamba binadamu hukosea na anahitajika kusamehewa, kama ndoa haita weka msamaha kama ngao yao, mhimili wa ndoa hii upo matatani.
MAWAZO MGANDO
Katika ndoa wanawake wengi huwategemea wanaume katika kutafuta na hata wengine wakijiita ni wanawake wa nyumbani, pia kuna wanaume wanaolelewa, ndoa haiwezi kuendelea kama hapatakuwa na maendeleo maana mtapata watoto na kipato toka uchumba hadi watoto watatu hali ni ile ile mwisho wa siku ndoa huvunjika kisa kipato shida.

Mwanandoa kutumia njia mbadala (wizi, uzinzi n.k), kwa mwanamke epuka kuwa mke wa nyumbani na mwanaume atafute kazi, hii pia husaidia katika tendo maana wote mnakuwa mmechoka tendo mnafanya kutafuta usingizi, vinginevyo ndio mchepuko unapoanzia. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top