Tatizo la ukosefu wa ajira ni suala ambalo limeendelea kuwatesa vijana wengi wa Kitanzania, licha ya takwimu za uchumi kwa mwaka jana kuonesha kukua kwa wastani wa asilimia 7.1 na kufanya vizuri katika kipindi cha muongo mmoja uliopita  ingawa umasikini haujapungua kama ilivyotegemewa na Watanzania.
Lazima ujue kuwa sio kweli kwamba mtaji pekee ndio kikwazo, lakini wengi wanaamini mtaji  ndio unawazuia. Lakini pia wakati huo ambao mtu hana mtaji hakuna juhudi anazofanya kuhakikisha anapata mtaji huo.
 
Sasa JIONGEZE na biashara hizi tano unazoweza kuanza kuzifanya bila ya kuanza na mtaji wa fedha.
Biashara ya uwakala wa mauzo (salesman)
Kuna makampuni mbalimbali ambayo yanatumia mawakala kuuza bidhaa au huduma zao. Kwa wewe kujifunza na kuwa wakala wao unaweza kupata kipato kizuri kwa njia ya kamisheni.
Biashara ya mtandao (Network marketing)
Hii ni biashara ambayo ni mkombozi kwa mtu yeyote ambaye ana kiu ya kufikia mafanikio. Hapa Tanzania kuna makampuni mengi yanayofanya biashara hii kama Forever Living, Oriflame, GNLD, na mengineyo. Katika makampuni haya kuna ambayo unaweza kuanza na kiasi kidogo cha fedha ambacho ni sawa na bure.
Biashara ya ushauri
Je kuna kitu ambacho una utaalamu nacho? Je kuna kitu ambacho unapenda kukifuatilia na hivyo unakijua sana? Vizuri, kuna mtu anataka kukijua ila hajui aanzie wapi. Kama wewe mmoja wa wanaoweza kutoa ujuzi na uzoefu kwa wengine unaweza kulipwa fedha.
Biashara ya taarifa (internet marketing)
Hii ni biashara ya kutoa taarifa kwa kupitia mtandao wa intaneti. Unaweza kuwa na ‘blog’  ambayo ni bure kuiendesha na baadaye ukaanza kupata kipato kizuri kupitia matangazo.
Biashara ya udalali
Hii ni biashara ambayo wewe unamsaidia mtu kupata kitu anachotaka na hana muda au uzoefu wa kukipata. Kama ukiweza kuifanya biashara hii kwa mbinu nzuri unaweza kutengeneza kipato kizuri.

Kumbuka; Biashara hizi zinahitaji ubunifu na kujituma tena kwa bidii na maarifa ingawa unaweza usione faida au mafanikio mapema. Ila ukiweka malengo na mipango mizuri utaona mafanikio makubwa baadaye. Uzuri ni kwamba unaweza kuanza biashara hizi ukiwa bado umeajiriwa au upo masomoni. 
JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top