Image result for Matumizi Ya (mabaya) Hovyo Ya Fedha
Tatizo kubwa linalozuia watu wengi kudhibiti matumizi ya kipato ni tabia yao ya kufanya matumizi ya kujionyesha kwa watu, au kuigiza maisha ambayo hawana uwezo nayo. Hili linaendelea kuwagharimu watu wengi sana, kama utaendelea kuishi maisha hayo kuwa na hakika utaendelea kuona kipato hakitoshi, na zaidi utaendelea kujikita katika madeni yasiona na umuhimu.
  
Tofauti iliyopo kati ya maskini na tajiri, ni namna wanavyofanya matumizi ya fedha zao. Maskini yeye hutumia kila fedha anayoipata lakini tajiri yeye hutumia kiasi cha fedha na kiasi huhifadhi kama akiba, na akiba hiyo, huwasaidia kuwekeza ili kutengeneza fedha nyingine zaidi.  
Image result for Matumizi Ya (mabaya) Hovyo Ya Fedha
Hebu leo tuangalie njia ambazo unaweza kuzitumia ili kudhibiti matumizi ya hovyo ya fedha:-

Jifunze kutumia  bajeti kuongoza matumizi yako. 
Bajeti huwa ni muongozo wa matumizi yako katika kipindi fulani cha muda. Usipokuwa na bajeti, utakuwa kama mtu ambaye anabahatisha katika matumizi yake, maana chochote kitakachoonekana mbele yake lazima kitamvutia na kukinunua. Utafiti unaonyesha kuwa aslimia zaidi ya 50, ya matumizi ya fedha za watu wa kawaida, huelekezwa katika matumizi ya vitu visivyo na umuhimu.


Tembea na fedha kidogo. 
Jitahidi sna kujenga tabia ya kutembea na fedha kidogo, au fedha za kile unachokwenda kununua tu. Acha fedha nyingine nyumbani au jifunze kuweka fedha eneo ambalo si rahisi kulifikia kwa haraka. Hii itakusaidia kutokufanya yale matumizi ya shinikizo.

Jipe muda kidogo kabla ya kununua kitu. 
Unapojipa  muda zaidi wa siku hata moja kabla kufanya manunuzi ya kile ulichotaka kununua itakusaidia kujitathimini kweli kama ulichokihitaji kukinunua kina umuhimu wowote kwako. Kwa sababu watu wengine wawapo na fedha huwa hawatulii wanatamani tu kufanya matumizi. 

Nunua kwa fedha taslimu. 
Jitahidi kujiwekea falsafa ya kununua kwa fedha taslimu tu, na kama huna fedha taslimu hutonunua chochote. Siku hizi biashara nyingi zina ushindani mkubwa sana, na baadhi ya wafanyabiashara hukopesha bidhaa zao kwa kipindi cha mienzi miwili, ili kukuvutia wewe. 

Hivyo unaweza kujikuta umeingia katika mtego wao, kukuvutia ukope; na usipokuwa makini utajikuta unalimbikiza madeni lukuki. Kumbuka madeni ni kikwazo kikubwa kuelekea kwenye uhuru wa kifedha.


 JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top