Image result for Wanawake wajawazito
Kama ulikuwa hujui basi jua kwamba Wanawake wajawazito wanashauriwa kulala kwa upande na sio kulala chali katika miezi mitatu ya mwisho ya ujauzito  ili kupunguza hatari kubwa ya kujifungua watoto waliofariki tumboni.
Hii ni Kutokana na Utafiti uliofanywa nchini Uingereza Imeelezwa kuwa wajawazito wengi wanapendelea kulala kwa mgongo (chali) jambo ambalo lina madhara makubwa sana hasa  kwa mtoto tumboni hata kuweza kusababisha kifo.
Utafiti huo umeonesha takriban mimba 225 nchini Uingereza huharibika na kwamba takriban maisha ya watoto 130 kila mwaka huokolewa kwa wajawazito ambao hulala kwa kutumia upande wa kulia ama kushoto.

 JIUNGE NASI KWA KUTUFOLLOW
fb@edonetz  , twiter@edonetz  , inst@edonetz_blog  na  youtube@edone tv
 
Top